Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 8, 2018

Wamiliki wa viwanda mikocheni wapewa mwezi

Wamiliki Viwanda Mikocheni wapewa mwezi mmoja Uhakika media 5  · 2 hours ago WAMILIKI wa viwanda eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam wamepewa mwezi mmoja kutatua kero ya uchafuzi wa mazingira kwa kudhibiti utiririshaji wa majitaka unaohatarisha afya za wakazi wanaoishi kabla ya kuchukuliwa kwa hatua kali za kisheria.  Agizo hili lilitolewa jana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi Lugola, baada ya kutembelea viwanda vya Iron and Steel Ltd na MMI Integrated Mills Ltd vilivyopo maeneo ya Mikocheni ‘B’ kujionea uchafuzi wa mazingira.  Akizungumza mara baada ya ziara yake ya ghafla, Lugola alisema hakuridhishwa na namna viwanda hivyo vinavyolinda mazingira na afya ya wananchi, hivyo kutoa mwezi mmoja kurekebisha hali hiyo.  “Nawaagiza wamiliki wa viwanda hivi wakutane na watendaji wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) mara moja kujadili namna ya kudhibiti uchafuzi wa mazingira, utirirshaji wa maji machafu, moshi n

Ashikiriwa na polisi kwa kumuua mwanaye

Ashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua mwanae kwa kumchapa na fimbo Uhakika media 5  · 1 hour ago Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Pader, nchini Uganda, linamshikilia Bwana Omony Odokonyero (30) kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mwanae mwenye umri wa miaka saba kilichotokana na kuchapwa  fimbo. Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor limeripoti Juni 7 2018, katika kijiji cha Omakigira, ambapo mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Richard Odokonyero, mwanafunzi wa shule ya msingi Pader Ogom alipigwa na fimbo baada ya kukataa kwenda shule akitaka kupelekwa kwa bibi yake. Mwenyekiti wa Kijiji hicho Charles Lalobo, amethibitisha tukio hilo na kudai kuwa mzazi huyo amekuwa na tabia ya kumpiga mtoto wake mara kwa mara na siku ya tukio alikuwa akimpiga na fimbo kichwani  hivyo kupelekea kuzimia kabla ya kufariki “Hili ni tukio ambalo halikupaswa kutokea, kuna njia nyingi za kutumia kama mzazi ili kufundisha watoto wao lakini sio kutoa athabu kali, Polisi wanapaswa kuchukua ha

Magazeti ya Leo 8/6/2018

MAGAZETI YA LEO 8/6/2018 Uhakika media