Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi 26, 2018

KADINARI PENGO APINGA WARAKA WA MAASKOFU WA KKKT

Mwadhama Kadinali Polycarp Pengo aukana Waraka wa Pasaka wa Maaskofu wa Kanisa katoliki Uhakika media 5  · 40 minutes ago Mwadhama Kadinali Polycap Pengo amesema hakuwa anajua kama kuna waraka utatolewa kuhusu kwaresma na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania huku akisema waraka huo una mazuri mengi japo umechanganya dini na siasa. Kadinali Pengo ameyasema hayo wakati akiadhimisha ibada ya Jumapili ya matawi huko Bagamoyo katika tamasha la vijana. "Katika wiki chache zilizopita watu wamekuja kwangu wakaniuliza unaionaje ile barua ya Maaskofu kuhusu Kwaresma mwaka huu? Ninazungumzia hilo na wala mtu asiende aka-quote kitu kingine ndio maana nataka kusema wazi kabisa:- "Barua ile ijapokuwa hata jina langu mnaliona limeandikwa pale kwamba na mimi ni mmoja wa waandishi au watamkaji...mimi nimeipokea, baadhi yenu mmeshaipokea. " Kwahiyo sioni namna gani mimi naweza kuwa mwandishi au mhubiri kwenu wa ile barua ambayo imetungwa labda na maaskofu...naamini na baad
MAGAZETI YA LEO 26/3/2018 Uhakika media · 2 hours ago

MAGAZETI YA LEO 26/3/2018

MAGAZETI YA LEO 26/3/2018 uhakika media  · 2 hours ago

RATIBA YA WIKI IJAYO KATIKA LITRUJIA YA KANISA TAKATIFU

KWA AMBAO HAWAJUI RATIBA YA WEEK IJAYO KATIKA LITRUJIA YA KANISA IPO HIVI :- Posted by uhakika media KESHO J3: Ni siku ambayo Yuda anajitoa maalum kabisa kwenye Jumuiya Ya mitume na anaanza mpango wake Kabambe wa kumuuza Yesu. J4:- Ndio siku ambayo Yuda atatimiza mpango wake na atakabidhiwa vipande 30 vya Fedha. J5:- Yesu anawatangazia Mitume wake mpango wa Yuda Japo kwa mafumbo na anaeleza waziwazi yale yatakayompata. Alhamisi :- Usiku, Yesu anaweka Sakramenti 3.      1. Kitubio.      2. Upadre.      3. Ekaristi Takatifu. Ijumaa :- Alfajiri Yuda anapokea kikosi chá Askari tayari kumsaliti Bwana wake, Mwalimu na Muumba wake. Hapa naomba niseme kidogo, kwa tamaduni za Waisraeli kulikuwa na Salamu za Mabusu za aina 3.    i. Salamu ya Bwana na mtumwa ambapo mtumwa alitakiwa kulala kifudifudi na kubusu miguu ya Bwana wake.   ii. Salamu ya Mwalimu na Mwanafunzi wake, ambapo Mwanafunzi alipaswa kupiga goti moja na kubusu mkono au mikono ya Mwalimu wake. Na hii ndio salamu am