Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 9, 2018

Waziri- Huduma usafishaji figo ni bure

Waziri - Huduma usafishaji figo ni bure Uhakika media 1  · 1 hour ago WAZIRI wa Afya Hamad Rashid Mohammed  amesema huduma za kitengo cha usafishaji figo  kwa wagonjwa wenye matatizo hayo katika Hospitali ya Mnazi Mmoja zinaendelea kufanyika  bila ya malipo yeyote .  Hayo aliyasema huko katika Hospitali ya Mnazi Mmoja wakati alipokuwa akifanya ziara ya kukagua kitengo hicho  na kuona jinsi kinavyoendelea na huduma zake    zinazofanyika katika sehemu hiyo kwa kuhudumia wagonjwa  kama kawaida.  Alisema lengo la ziara hiyo ni kuona jinsi wananchi wanavyofaidika na huduma hiyo  kwani Serikali inataka wananchi wake wasihangaike kutafuta huduma hiyo  kwa kuifuata nje ya nchi au masafa marefu.  Aidha alisema Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuwajali wananchi wake  imekuwa iko imara katika kuhakikisha inakipa kipaumbele kwa kukipatia vifaa vyote  pamoja na dawa  za kusafishia mafigo.  “Wananchi mnapofikwa na matatizo haraka fikeni Hospitalini ili muweze kupata huduma dawa zipo za kut

Waweza kabisa kuwa daktari

WAWEZA KABISA KUWA DAKTARI Soma hapa Uhakika media 1 hour ago St. David college of health kimara temboni ni chuo pekee tanzania kinacho kupa fursa ya ndoto yako ya kuwa daktari bingwa.  ANZIA HAPA:   Uwe na ufaulu wa PCB  Physics Chemistry Biology.......angalau kwa alama D tu.. Mfumo umebadilika wa kudahili wanafunzi, sasa omba chuoni moja kwa moja badala ya kwenda NACTE. Pia ufaulu wa Hesabu na kiingereza ni sifa ya ziada /nyongeza sio ya lazima.  Ada ni nafuu mno na pia waweza soma kwa uwezo wa shughuli zako, Wasiliana nasi  0654 354949 / 0716044610 / 0718229977  

VIDEO:Samatta, Joti, Julio watamba wataja kikosi Kiba kitakacho wapiga timu Kiba

VIDEO: Samatta, Joti, Julio watamba wetaja kikosi kitakachowapiga timu Kiba Uhakika media minutes ago Kuelekea Mechi itakaoyopigwa mda mchache kuanzia sasa kwenye uwanja wa taifa kati ya timu Kiba na Samatta, Joti ametaja kikosi kitakachoivaa timu Kiba huku akiahidi ushindi. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI .......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Katibu mkuu wa UWT aahidi makubwa CCM

Katibu Mkuu wa UWT aahidi makubwa CCM Uhakika media 1  · 46 minutes ago Katibu Mkuu wa Umoja wa wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), Ndugu Queen Mlozi ameahidi kufanya kazi kwa weledi, uaminifu na uzalendo uliotukuka ili CCM ishinde katika uchaguzi mkuu wa dola mwaka 2020.  Hayo ameyasema wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa ngazi mbali mbali za UWT Zanzibar hapo Afisi Kuu CCM Kisiwandui katika ziara yake ya kwanza kujitambulisha kwa viongozi na watendaji hao.  Alisema atatekeleza majukumu yake kwa ufanisi kwa lengo la kuimarisha taasisi hiyo ili kwenda sambamba na kasi ya maendeleo ndani ya Umoja huo na Chama kwa ujumla.Ameeleza kwamba wanawake wa UWT wanatakiwa kuelekeza nguvu zao katika kulinda maslahi ya CCM ili ishinde kwa ngazi zote kwa upande wa Tanzania bara na Zanzibar katika uchaguzi Mkuu ujao.  Katibu Mkuu huyo amewashukuru viongozi viongozi wote wa Chama Cha Mapinduzi waliomuamini na kumteuwa kushika nafasi hiyo ya ngazi ya juu ya kiutendaji kupi

TRA. Wananchi acheni kufanya biashara za magendo

TRA - Wananchi acheni biashara za magendo Uhakika media 1  · 41 minutes ago Wito umetolewa  wanakijiji cha Kigombe Kata ya Kigombe wilayani Muheza mkoani Tanga kuacha kushiriki kwenye biashara za magendo badala yake watumie maeneo yaliyorasmi kisheria kwa ajili ya upitishaji wa bidhaa.  Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo wakati akizungumza na wananchi  kwenye mkutano uliofanyika eneo la sokoni akiwa ameambatana na maafisa wa TRA Mkoani Tanga.  Alisema kitendo cha wananchi kuacha kutumia bandari ya Pangani ambayo ipo kisheria wanafanya makosa makubwa na kuwataka kuitumia kupitisha bidhaa badala ya kutumia zile ambazo hazitambuliki ambazo watakapokamatwa watafikishwa kwenye vyombo vya kisheria.  “Tumefika hapa kigombe kutoa elimu kwa kuzungumza na wananchi kutokana na changamoto za mara kwa mara biashara za magendo ambazo zimekuwa zikipitishwa eneo hilo na kuona kutumia muda huo kuzungumza na wan

Magazeti ya leo 9/6/2018

MAGAZETI YA LEO 9/6/2018 Uhakika media  3 hours ago

Serikali yaingilia kati tukio la mwanamke kujifungulia nje ya kituo cha polisi

Serikali yaingilia kati suala la Mwanamke kujifungulia nje ya Kituo cha Polisi Uhakika media 5  · 4 hours ago Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya askari polisi waliosababisha mwanamama Amina Rafael kujifungua nje ya kituo cha Polisi cha Mang’ula huko mkoani Morogoro.  Kauli hiyo ya Masauni imekuja baada ya kutakiwa kutoa maelezo na Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kuhusiana na madai hayo yaliyotolewa na Mbunge wa Arumeru Mashariki , Joshua Nassari aliyetaka suala hilo lijadiliwe ndani ya Bunge na kwamba ni matukio yanayoendelea kujitokeza ikiwamo Dar es Salaam, Tarime na Mwanza.  Naibu Waziri Masauni amesema, serikali imesikitishwa na suala hilo na tayari jalada la uchunguzi limeshafunguliwa.  Akielezea tukio hilo Masauni amesema "kulikuwa na tukio la wizi, lililomhusisha mume wa huyu mama, (Abdallah Mohamed), anayedaiwa kununua vitu vya wizi ambavyo vilikutwa katika nyumba yake, Polisi walimtaarifu mama kwamba mu

Kigoma kujenga vizuizi kuzuia ajali

Kigoma kujenga vizuizi kuzuia Ajali Uhakika media 5  · 4 hours ago Serikali imesema itahakikisha inajenga Vizuizi katika maeneo ambayo Barabara imepishana na reli ili kudhibiti Ajali katika maeneo hayo na Magari yawe yanasimama wakati Treni ikipita.   Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Samson Anga ikiwa zimepita Siku mbili tangu kutokea kwa Ajali ya basi dogo lililogonga treni eneo la Gungu mkoani Kigoma na kusababisha vifo vya watu 10 na wengine 35 kujeruhiwa.  “Haiwezekani watu wapoteze maisha kwa sababu ya uzembe wa baadhi ya madereva. Tumechoka kuona hali hii ikiendelea na lazima tuchukue hatua kuokoa maisha ya binadamu wenzetu," amesema.   Amesema ujenzi wa vivuko utahusisha wakala wa barabara (Tanroads) na Shirika la Reli Tanzania(TRC) ambao wataratibu na kujenga vizuizi hivyo.  Maeneo ambayo reli imepishana na barabara mkoani Kigoma ni Kibirizi, Gungu, Nyamoli, Kazuramimba, Uvinza, Tubira na Malagalasi. 

CHADEMA Wanena mazito kwa wanachama wake

Chadema: Nataka kuwahakikishia watanzania kwamba CHADEMA iko imara kuliko jana Uhakika media 5  · 4 hours ago Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefunguka na kudai hakijawahi kushindwa uchaguzi wowote ule ambao umefanyika katika ardhi ya Tanzania bali kinachowapata ni kupokwa matokeo yao na kurundikwa katika chama kingine cha siasa. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA),  Patrick Ole Sosopi wakati alipokuwa anazungumza kwenye media tour yake leo Juni 08, 2018 Jijini Dar es Salaam na kusema ushahidi wa jambo hilo ni mmoja wapo ni uchaguzi wa mdogo wa marudio katika Jimbo la Kinondoni ambapo sanduku la kuwekea kura liliibwa mbele ya askari polisi na likarudishwa huku kukiwa hakuna mtu yoyote aliyekamatwa. "Nataka kuwahakikishia watanzania kwamba CHADEMA iko imara kuliko jana, kuzuiwa kwa mikutano ya kisiasa ndio inaathari kwa sababu kazi yetu ni siasa,upande wa pili anatuimarisha zaidi sababu nyuma ya pazia kila mtanzania an

Chuo cha Royal Collage na vingine 20 vyafungiwa NACTE

Chuo cha Royal College na vingine 20 vyafungiwa na Nacte Uhakika media 5  · 4 hours ago Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte) limefuta usajili wa vyuo 20 baada ya kushindwa kufuata sheria zinazoendana na matakwa ya usajili wa vyuo hivyo.  Akizungumza leo Juni 8, Kaimu Katibu Mtendaji wa baraza hilo Dk Adolf Rutayuga amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kufanyika kwa ukaguzi wa vyuo 458 na 32 vilikutwa na mapungufu.  Sanjari na 20 vilivyofungiwa vyuo tisa vimezuiliwa kudahili wanafunzi wapya huku vyuo vitatu vikitakiwa kusitisha baadhi ya kozi walizokuwa wakitoa bila idhini ya baraza.  Dk Rutayuga amesema tayari baraza hilo limeshaviandikia barua vyuo 20 vilivyofungiwa kuvitaka vihakikishe kuwa wanafunzi wanahamia kwenye vyuo vingine.  Vyuo vilivyofutiwa usajili ni Royal College, Covenant College of Business Studies,  Mugerezi Spatial Technology College, Techno Brain, Lisbon Business College, PCTL Training Institute na Mlimani School of Professional Studies vyote vya Dar es

Yanga yaikwepa simba Kagame

Yanga waikwepa Simba, Kagame Uhakika media · 3 hours ago Tetesi zinaeleza kuwa uongozi wa klabu ya Yanga imeiandikia barua Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF), kuwaomba kujitoa katika mashindano ya Kagame CUP yanayotarajiwa kuanza June 28 mpaka Julai 13 2018 jijini Dar es Salaam.  Sababu za msingi ziliifanya Yanga kuandika barua hiyo ni kufanya maandalizi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika ambapo watacheza na Gor Mahia FC ya Kenya, Julai 18 jijini Nairobi.  Kutokana na muingiliano wa ratiba ya KAGAME na CAF, Yanga wameona ni vema kuwapatia wachezaji wao mapumziko ili kuwapa fursa ya kujiandaa vizuri kuelekea mechi hiyo ambayo itakuwa ni ya tatu baada ya kucheza na USM Alger pia Rayon Sports ya Rwanda.  Eatv.tv imemtafuta Katibu wa klabu hiyo Boniphace Mkwassa ambaye amethibitisha kuwa Kamati ya Utendaji wa klabu, wameazimia kufanya maamuzi hayo ili kuepuka kubanwa na muingiliano wa ratiba hiyo ambayo imekuwa si rafiki kwao.  Kufuatia kuandika barua hiyo ya kuomba ku

Serikali yajibu mwanamke kujifungulia polisi

Serikali yajibu tukio la mwanamke kujifungulia Polisi Uhakika media 5  · 54 minutes ago Kufuatia tukio la mwanamke mjamzito kujifungua kwenye Kituo cha Polisi Mang’ula mkoani Morogoro, serikali imebanwa bungeni na kutakiwa kutoa ufafanuzi.  Hoja hiyo iliibuliwa na Mbunge wa Meru, Joshua Nassari ambapo alitaka kujua kwa nini mwanamke huyo mjamzito aliyekuwa akikaribia kujifungua alikamatwa na kuwekwa mahabusu na baadaye uchungu kumbana akiwa nyuma ya nondo kabla ya baadaye kutolewa na kujifungua nje ya kituo hicho.  Akitoa ufafanuzi, Naibu Waziri wa Ndani, Hamad Masauni, amekiri kwamba busara haikutumika katika sakata hilo kwani chanzo cha kukamatwa kwake ni mali za wizi zilizonunuliwa na mumewe kukutwa ndani ya nyumba yake. Waziri Masauni ameeleza kwamba serikali inafuatilia kwa kina na wote waliohusika watachukuliwa hatua zinazostahili.

Mbaroni kwa kuiba vifaa vya mama Samia

Mbaroni kwa kuiba vifaa vya Mama Samia Uhakika media 3  · 50 minutes ago Jeshi la polisi mkoani Dodoma limeendesha msako na kukamata watuhumiwa 19 kwa makosa mbalimbali ya uhalifu ikiwemo watuhumiwa wa uvunjaji walioiba vifaa vya mafunzo ya TEHAMA vilivyotolewa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan vyenye thamani ya zaidi ya  shilingi Milioni 56 ambapo vifaa hivyo vilitolewa kwa ajili ya mradi maalum wa mafunzo ya tehama nchini  Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa polisi Gilles Muroto amesema msako huo umekamata watuhumiwa wa makosa ya uvunjaji,watuhumiwa wa kusafirisha madawa ya kulevya pamoja na watuhumiwa wa utapeli ambapo amesema watuhumiwa hao watafikishwa mahakama kujibu tuhuma zinazowakabili.  Aidha katika hatua nyingine Kamanda Muroto amewataka wananchi kutii sheria bila shuruti na kutoa taarifa za wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu ambapo amesema mkoa wa Dodoma ambao ni makao makuu ya nchi hautowavumilia wanaojihusisha na uhalifu.  ITV im

Wizara ya maliasili yafanikiwa kutatua migogoro

Wizara ya utalii yafanikiwa kutatua migogoro Uhakika media 3  · 46 minutes ago Serikali imesema imeweka mpango kabambe wa kuhakikisha vituo vyote vya utalii vilivyopo hapa nchini  vinatangazwa ili viweze kulinufaisha taifa.  Naibu Waziri wa mali asili na utalii Japhet Hasunga amesema hayo bungeni mkoani Dodoma wakati akijibu maswali yaliyoelekezwa kwa wizara hiyo.  Amesema kupitia mkakati huo Wizara hiyo inahitaji ushirikiano wa jamii kuweza kuwaeleza viongozi wa maeneo yao kuhusiana na vivutio vilivyopo maeneo yao ili viweze kutambulika.  Aidha naibu Waziri Hasunga ameliambia bunge kuwa wizara hiyo ya mali asili na utalii imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutatua migogoro iliyokuwepo kati ya wananchi waishio jirani na hifadhi na hifadhi husika.

Vyuo vilivyo futwa vyapewa nafasi nyingine ya usaili

Vyuo vilivyofutwa vyapewa nafasi nyingine ya usaili Uhakika media · 36 minutes ago Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limefuta usajili wa vyuo 20 kwa kushindwa kufuata utaratibu wa usajili wa vyuo vya ufundi na upungufu wa rasilimali za kufundishia. Kaimu Katibu Mtendaji wa NACTE, Dkt. Adolf Rutayuga amesema vyuo hivyo bado vina nafasi ya kuomba usajili upya endapo watarekebisha matatizo na utaratibu ukafuatwa. “Matokeo ya uchunguzi uliofanywa kuanzia Julai 2017 mpaka Septemba 2017 ambao ulihusisha vyuo 458 ambapo 112 vya ualimu na vingine 7 vilivyokutwa haviendelei na shughuli za elimu, vyuo 426 vimekidhi vigezo lakini vyuo 32 vimekutwa na mapungufu hivyo Baraza limechukua hatua mbalimbali kwa vyuo hivyo 32,”  Dkt.  Rutayunga. Pia Baraza limezuia vyuo 9 kudahili wanafunzi wapya kwa mwaka wa masomo 2018/19 na vyuo 3 vimesitishwa kutoa program zisizohidhinishwa na Baraza hilo.

Kocha wa uholanzi awalipa wachezaji mshahara

Kocha wa Uholanzi awalipa wachezaji mishahara Uhakika media. · 30 minutes ago Kocha wa timu ya taifa ya Australia Bert van Marwijk, ameamua kuwalipa mishahara makocha wenzake kwenye benchi la ufundi la timu hiyo, ambayo imefuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi.  Marwijk ambaye ni raia wa Uholanzi amefikia uamzi huo baada ya chama cha soka nchini humo kumgomea kumpa bajeti ya kuongeza wataalam kwenye benchi lake kutokana na ukosefu wa pesa za kuwalipa makocha hao.  Hata hivyo yeye amedai ameamua kufanya hivyo kwasababu anataka timu ifanye vizuri na hivyo ndio taaluma yake inamtaka afanye, bila kujali malipo huku akiongeza kuwa hata hao aliowachukua wanajali zaidi suala la taaluma na sio malipo.  ''Kwenye kitu chochote kinachohitaji mafanikio hususani kwenye taaluma lazima malipo yawe kitu cha mwisho lakini weledi uanze mwanzo na ndio kinafanyika hapa, tunataka tufanye vizuri Urusi na hiyo itatupa fursa nyingi sisi'', amesema.  Van Marwijk aliteu