Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka
 
Kipanda uso ni ugonjwa gani?
 
Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.
 
Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.
 
Dalili za Kipanda Uso:
 
Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile;
1. Kujisikia uvivu,
2. Kutapika,
3. Mauzauza,
4. Kusikia kelele sikioni nk.
Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk
Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na:
1. Mfadhaiko wa akili (stress)
2. Kelele nyingi kuzidi
3. Kuluka kula mlo
4. Pombe
5. Sigara
6. Shinikizo la chini la damu
7. Kutokunywa maji mengi kila siku
8. Kukosa usingizi
9. Aleji
10. Harufu kali
11. Mkao mbovu 
12. Kubadilikabadilika kwa homoni.
 
Wapo watu haiwezi kupita wiki bila kunywa aina fulani ya dawa kutuliza maumivu ya kichwa au kipanda uso. Hata hivyo matumizi hayo ya mara kwa mara ya hizo dawa mwishowe huleta madhara makubwa katika afya.
 
Kwahiyo, kwanini sasa usijisomee hapa na ujipatie ufahamu juu ya dawa za asili za kuondoa maumivu ya kipanda uso zisizo na madhara yoyote baadaye?
 
Endelea kusoma …
Kipanda uso
 
Kipanda uso na tiba yake:
 
Hizi ni dawa mbadala au dawa asili 8 unazoweza kuzitumia unapopatwa na kipanda uso ili kuondoa maumivu hayo na hatimaye kupona kabisa:
 
Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka
 
1. Siki ya tufaa na asali
“Siki ya tufaa ni moja ya dawa za asili zenye viinilishe vingi mhimu kwa afya..”
 Pamoja na mengine mengi unaweza kutumia siki ya tufaa kujitibu na matatizo kama kisukari, kutibu kipanda uso, kupunguza maumivu ya mifupa na kuondoa tatizo la kufunga choo. Kwahiyo kwanini usiijaribu siki ya tufaa kutibu kipanda uso chako?
Tumia kwa kufuata maelezo yafuatayo:
 
a) Weka kijiko kimoja cha siki ya tufaa ndani ya kikombe kimoja cha maji (robo lita)
b) Ongeza asali kijiko kimoja
c) Changanya vizuri
d) Kunywa mara moja mchanganyiko huu kwa siku mara 1 ili kutibu kipanda uso.
Unatakiwa uendelee kutumia dawa hii kwa majuma kadhaa mpaka umepona.
 
Muda wowote ukipata maumivu ya kipanda uso tena unaweza kuchukua vijiko viwili vya siki ya tufaa na unywe kupunguza hayo maumivu.
 
2. Kipande cha barafu
 
Pengine kutumia kipande cha barafu ndiyo dawa rahisi zaidi ya asili ya kutibu kipanda uso. Itakusaidia kupunguza maumivu yatokanayo na kipanda uso. Unapotaka kutumia kipande cha barafu kutibu kipanda uso fuata njia hizi:
 
a) Tumia kitambaa safi na ufunge kipande cha barafu katika hiki kitambaa
b) Weka barafu ndani ya kitambaa ukipitisha pole pole kwenye paji la uso na shingoni kwa dakika 15 hivi
c) Fanya zoezi hili kila unapotokewa na maumivu ya kipanda uso
 
3. Pilipili kichaa na limau
 
Pilipili kichaa ni dawa nzuri ya asili pia kwa kutibu kipanda uso. Inaweza kuongeza wingi na msukumo wa damu mwilini. Vile vile hutumika kutibu hata kuondoa maumivu mengine ya kawaida ya mwili.
Hivyo ikikutokea kipanda uso fuata njia hizi kwa kutumia pilipili kichaa na limau:
 
a) Chukua nusu kipande cha pilipili kichaa na uweke ndani ya kikombe kimoja cha maji ya moto.
b) Changanya vizuri
c) Ongeza kidogo asali au maji maji ya limau ndani yake
d) Kunywa maji hayo kutwa mara 1 ili kutibu kipanda uso kinapokutokea
 
4. Chai ya Tangawizi
 
Tangawizi ni dawa nyingine ya asili ya kutibu kipanda uso. Tangawizi inaondoa uchovu, inasaidia kuweka sawa homoni, husaidia kutanuka kwa misuli na kuondoa maambukizi kwenye mishipa ya damu.
 
Kwahiyo mara upatwapo na kipanda uso jaribu kufuata njia ifuatayo ukitumia tangawizi kujitibu kipanda uso:
 
a) Tengeneza chai ukitumia tangawizi freshi (mbichi) na unywe kikombe kimoja mara 2 au 3 hivi kwa siku. Usiweke majani ya chai humu.
b) Au wakati mwingine maumivu ya kipanda uso yakikujia chukua kipande cha tangawizi mbichi na utafune. Itakuondolea hayo maumivu na uchovu pia.
 
5. Mafuta ya ufuta na unga wa mdalasini
 
Unapopatwa na kipanda uso au hata maumivu ya kawaida ya kichwa dawa nzuri kabisa ni kufanya masaji ya kichwa. Kufanya masaji ya kichwa kutasaidia kutibu kipanda uso sababu masaji inaziba ishara za maumivu zinazotumwa kwenda kwenye ubongo.
 
Masaji pia inaongeza ufanisi wa kazi wa homoni iitwayo ‘serotonin’ ambayo inahusika na kuweka utulivu wa akili na kukupa usingizi. Kwahiyo utakapopata kipanda uso tena fanya yafuatayo:
 
a) Chukua vijiko vikubwa viwili vya mafuta ya ufuta na uyapashe kidogo katika moto
b) Changanya na nusu kijiko kidogo cha unga wa mdalasini na nusu kijiko kidogo kingine cha iliki ya unga ndani ya mafuta ya ufuta
c) Pakaa mchanganyiko huu kwenye paji lako la uso
d) Jimasaji pole pole
e) Acha hivyo kwa lisaa limoja hivi
f) Jisafishe na maji ya uvuguvugu
Fanya zoezi hili kutwa mara 1 kila siku mpaka umepona
 
6. Tufaa (Apple)
 
“Tunda moja la tufaa kwa siku linatosha kuondoa uhitaji wa daktari.”
 
Kula matunda ni afya au ni jambo zuri kwa afya yako. Matunda ya tufaa (au epo) ni matunda yenye viinilishe mhimu sana kwa ajili ya mwili kiasi kwamba ukiwa na tabia ya kula tunda hili moja tu kwa siku hutakuwa na hitaji lolote la kuonana na daktari.
 
Tufaa ni tunda maarufu sana duniani na lina faida nyingi zinazoweza kutumika kutibu maradhi mengi. Mara tu unapopatwa na maumivu ya kipanda uso kwanini usijaribu kula tufaa? Unachotakiwa kufanya ni kula tu hili tunda mara tu unapopatwa na maumivu ya kipanda uso.
 
Kitendo hiki cha kula tu hili tunda kitakuondolea hayo maumivu na baadhi ya tafiti zinasema ukinusa tu ganda la kijani la tufaa inasaidia pia kupunguza maumivu ya kipanda uso.
 
7. Kahawa na Limau
 
Kahawa ina kaffeina ambayo inaweza kuziba baadhi ya vipokezi na mishipa ya damu kutuma ishara au ujumbe wa maumivu katika ubongo. Kwahiyo kikombe kimoja cha kahawa kinaweza kukusaidia kuondoa maumivu ya kipanda uso.
 
Kwahiyo wakati utakapopata kipanda uso kunywa kikombe cha kahawa na ukihitaji matokeo mazuri zaidi basi ongeza kijiko kidogo kimoja ndani yake cha maji maji ya limau.
 
Mhimu tafadhali: Pamoja na kuwa kahawa inaweza kutumika kwa ajili hii kama dawa ya kutuliza kipanda uso bado nakuonya usizidishe matumizi ya kahawa kwani kaffeina iliyomo kwenye kahawa ina madhara mengine mabaya kiafya ukizidisha kuitumia.
Hivyo kipanda uso chaweza kuongezeka zaidi kama utazidisha kunywa kahawa.
 
8. Chumvi
 
Chumvi pia ni dawa nzuri ya kutibu kipanda uso. Kama unataka kutumia chumvi kutibu kipanda uso fanya hatua zifuatazo:
 
a) Andaa maji ya kuoga ya moto
b) Weka chumvi kikombe kimoja au viwili (chumvi ya mawe ndiyo nzuri zaidi)
c) Tumbukiza mwili wako wote ndani ya haya maji kwa dakika 15 hivi na utulie.
d) Hii itakuondolea au kuzuia maumivu wakati ukipatwa na kipanda uso.
 
Maumivu yakizidi muone daktari.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am