Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1
Uhakika media

SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA

Mwandishi: SEID BIN SALIM

SEHEMU YA KWANZA
Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale.

waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke yao, lakini namna siku zilivyozidi kwenda ndivyo lucky alizidi kutia huruma na kuishi katika mazingira ya kuusononesha uso wake, uvumilivu uliwashinda na kuamua kumkalisha chini ikiwezekana awaambie chochote kinachomsumbua moyoni mwake uenda wakawa na ushauri wa kumshauri.

" Lucky mpenzi, kikao hichi ni kwa ajili yako, tumeacha shughuli zetu ili tuongee nawe, tumeishi hapa mwaka sasa, lakini mwendo wako na wetu ni vitu viwili tofauti, kuna muda tumekushuhudia ukimwaga machozi bila sababu, mawazo yasiyoisha, huzuni wasi wasi na vingine kama hivyo, kitu ambacho kimetushinda kiukweli, kwa sababu sisi wakati wote ni watu wa kufurahi, kucheka, kununa kukasirika hatujui. so tunaumia sana tunapoona mwenzetu tunaeishi nae chumba kimoja hauko kama sisi, huoneshi furaha hata siku moja, tunaomba utueleze kitu gani hasa kinasumbua maishani mwako tafadhali.. Tunu aliekuwa pembeni yake alimuuliza akiwa amemuangalia kwa kushika mkono kwenye tama, lucky mwenyewe alishikilia mto uliokuwa mapajani mwake, machoni akionesha hayuko nao, mariam na Amina walikuwa wamekaa katika kitanda cha pili wakimtizama kwa macho yasiyoisha huruma.

" tunaomba utuambie kitu gani kinakusumbua maishani mwako, sisi ni marafiki wema, au tokea uingie hapa kuna jambo lolote baya tumekufanyia linalokufanya uwe hivyo?. Aliuliza Tunu lucky akatingisha kichwa kuashiria hamna. sasa kwa nini unatufanyia hivyo hatupendi lucky, twambie nini kinakusumbua hatuitaji uwe katika hali hiyo.

" Hapana Tunu mimi sina tatizo lolote. Alisema baada ya kupitisha mkono machoni kutoa machozi yaliyokuwa tayari yanamlenga.
" Lucky unajaribu kuficha ugonjwa usiofichika, hapo tu tayari machozi yanakutoka kisha unasema huna tatizo, tuko wanne tu hapa, zaid yetu hakuna mwengine anaetuona wala kutusikia tuambie tafadhali.. alisema dada mwingine Mariam ambae walipendelea sana kumuita Baby Mimah.
" mtoto koma mwengine yupo anaetusikia. Amina Alidakia maneno ya mimah.
" Ushaanza nani anatuona hapa?. Aliuliza mimah kwa kushtuka, amina kidogo alikuwa shambenga asietaka kitu kimpite.
" Sir God, anaona hadi uvunguni kama hujui.
" nlijua tu utasema hivyo, usilete matani wakati tuko serious bhna, unaichukulia baridi hali ya mwenzetu eee?
" Hapana kazi na dawa, kucheka kidogo kununa kidogo maisha yanaenda, bby lucky tunaomba utuambie basi kitu gani kinakusumbua mamy, ujue kukaa na tatizo moyono si kutatua tatizo ee. Alisema Amina.
" Sina tatizo mimi Amina niko kawaida.
" tatizo unalo, ujue hapa chuoni kuna kamchezo kabaya kanaendelea japo kwa upande mwengine kazuri, tukikuona hivyo hatukuelewi tutaenda kushtaki kwa calacte., so bora utuambie sisi mpenzi umbea utabaki humu humu ndani. Alisema amina huku akiwa amewaangalia wenzake.
" nawaomba hali yangu msimwambie mtu yoyote, siitaji watu wajue nnavyoishi, haya ndo maisha yangu tokea niko nyumbani. Alisema lucky akiwa ameangalia chini, waliendelea kumshawishi ili awaambie kile walichokuwa wanakiisi tokea kwake lakini wapi, mwisho waliamua kuachana nae wakimsihi sana abadilike laa sivyo watashindwa kuishi nae, upweke anaoweka hawauwezi kutokana na jinsi walivyozoea kucheka na kila mmoja..
Siku zilisonga mbele maisha ya lucky yakiwa hayo hayo ya ukimya muonekano wa msongamano wa mawazo na kujipwekesha na wenzake, ilifika sehemu wenzie anaolala nao walichoka ikabidi wamfate tena kumuweka chini lakini hakuna kilichobadilika, jinsi alivyokuwa anakaa alifanana na msaka tonge anaesaka tonge lake katika wakati mgumu wakati anatoka moja ya familia za kitajiri mno jijini DAR ES SALAM..
alivyoishi chuoni hapo lucky ( UNIVERSITY OF DAR ES SALAM ) walimu wengi walitokea kumpenda na kumjumlisha ndani ya daftari la wanafunzi bora mfano wa kuigwa na kila mmoja, kipindi chote cha mwaka mzima alibahatika kupokea tuzo ya mwanafunzi msafi na mwenye nidhamu kuliko wote, hakuna alichoambiwa na walimu afanye akakataa labda kiwe kibaya, alikuwa mtiifu kuliko watiifu, upole huruma kwa wanafunzi wenziwe pamoja na muonekano wa kudel na masomo wakati wote hata alipokuwa chumbani.

Wengi walipendelea mambo ya michezo wanapokuwa hawana ratiba yoyote ya masomo, au kutumia muda huo kwenda kula bata sehemu mbali mbali maclub na kwengine, lakini yeye vitabu vilimkoma baadhi ya wanafunzi wakawa wanamuonea wivu, tabasam kwake ndo kilikuwa kicheko tofauti na wengine, hakuna alichokiitaji zaidi ya kusoma, pale alipochoka alipanda kitandani kulala, lakini moja ya kawaida yake ambayo anaolala nao waliizoea, hawez kulala mpaka machozi ya mawazo yamtoke, kitu kilichopelekea waamini uenda alipitia kipindi kigumu cha maisha ndo maana analia kila wakati.
Hakuna alieweza kujua kama lucky anatoka kwenye familia ya kitajiri sana uenda kuliko wanafunzi wote chuoni hapo, hakuwa akijionesha kuwa kwao uwezo upo tena mkubwa, alionekana mwanafunzi wa kawaida kuanzia mavazi, misuko ya nywele na vitu alivyokuwa anatumia.

Familia yake yote ilikuwa ikiishi pembezoni mwa jiji la dar masaki karibu kabisa na bahari ya hindi, mama yake aliejulikana kwa jina la jenipha alikuwa mganga mkuu katika hospitali ya mhimbili, kaka yake anaemfata alikuwa mmiliki wa makampuni matatu ya usafirishaji madini kwenda nje, huku baba yake mzee edwad akiwa mfanyabiashara mkubwa wa kimataifa..

Utajiri wa familia hii ulikuwa mkubwa mno kuliko hata wa viongozi waliokuwa madarakani. Iliishi kwa upendo muda wote, majirani waliiangalia kwa jicho la tatu namna inavyoishi, waliyatamani maisha yao wanayooneshana wakiwa nje, kitu kilichokuwa tofauti kwa mama mwenye nyumba jenipha aliekuwa anaiona bora jana kuliko leo, ila haikuonekana hivyo kwa majirani kwa sababu waswahili walishasema USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA KIZA..
Maisha ya chuo kwa lucky yalisonga mbele, maryam, Tunu na amina waliamua kumuacha kama alivyo wao wakaendelea na ya kwao, walimtoa thamani na kumuona mjinga asiejua kitu na uenda ametoka shamba ( kijijini) ndo maana anakuwa hachangamuki, ila lililokuwa moyoni mwake hakuna alieweza kulifahamu, na alikubali kuonekana mjinga mbele ya wanaojiona wajanja ili maisha yake yaweze kusonga mbele..

" Rafiki yangu namuonea huruma sana huyu mwenzetu, yani anaishi kama mtu wa kijijini kimandazi mandazi tu sijui yukojee,, msiiiiu. Asubuhi ya jumaa tatu lucky akiwa bafuni anakoga kujiandaa kuingia kwenye kipindi ambapo wao walishajiandaa, Tunu alisema na wenzake namna anavyomchukulia lucky kwa kipindi hicho mbali na nyuma alivyokuwa akimueshimu.

" Si bora mandazi hayachachi, ila Achana nae mshamba huyo, ukimuita haitiki, ukimsemesha anajibu shot, ukimuomba hiki mpaka atake, ana nini kwani hadi tumbembeleze bhana, uzuri wa kutuzidi hana, akituzidi sehemu nyingine tu lakini si face, tufanye yetu tumpoezee aishi kivyake. Alidakia amina.
" mi nlizani mnankalisha chini kusema vitu vya maana kumbe ni huyu chapati, achaneni nae bhana. Kila mmoja mzuri humu ndani na kila mtu nyodo anaziweza, ametunyodoa tumnyodoe, tena sasa hivi niwakupewa visa mpaka chumba akihame hiki. Twendeni class. Alidakia maryam. 

" hhhhhmmmmm. Aliguna tunu, kumbe na wewe umo?. Walinyanyuka na kicheko kila mmoja akabeba mkoba wake na kwenda darasani. lacky alitoka bafuni akiwa na khanga moja mwilini akakaa kitandani na kujifuta futa maji, hakukaa dakika akanyanyuka na kusogea kwenye kioo kujiangalia mwili wake wote ulivyo. Alivuta mafuta aina ya lotion akajipaka baadhi ya sehemu za mwili wake, alipomaliza aliitoa khanga mwili ukabaki utupu kisha akavaa nguo za ndani zilizokuwa kwenye henga.. 

Alimaliza kwa nguo za chuo akabeba mkoba na kutoka ndani, hadi anafika darasan hakuna alieweza kumpa hi kwa sababu ya kusikojulikana sana na watu, kwa alivyokuwa anajiweka hakuna aliweza kumzoea kwani hata mbinu ya kumuingia haikuwepo, wapo wanaume waliojifanya midomo mirefu kutaka kuingiza mistari ya kumtongoza kutokana na uzuri wa mvuto aliokuwa nao kuanzia sura hadi maumbile, lakini walijikuta wanashindwa na kujionea aibu namna ambavyo lucky hakutaka upumbavu..

NINI KITAENDELEA KATIKA EPSODE YA PILI 

Maoni

  1. Ndugu msomaji wa blog hii endelea kuwa nasi kwa ukaribu ili upate kujua mengi kupitia blog hii. Tunakuletea mambo mbalimbali pia unaruhusiwa kutoa maoni ni nini unapenda tukuletee humu.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am