Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NAMNA YA KUPATA PESA UKIWA NA BLOG YAKO

Unawezaje kupata pesa au faida kwa kumiliki blogu?
Published by uhakika media 
Unataka kutenegeneza pesa kirahisi sio?, bila shaka, kila mtu anataka kutengeneza pesa halali imsaidie kusukuma maisha yake ya kila siku. Pengine umewahi sikia kuwa ukimiliki blogu ama tovuti unaweza kutengeneza pesa kirahisi?, ndio yawezekana kutengeneza pesa kirahisi kwa kutumia blogu, ila usiwe na shauku sana maana si rahisi tu. Wasomaji wangu wengi wamenitumia ujumbe na wengine kunipigia simu kuuliza nawezaje kupata pesa nikiwa na blogu yangu? Leo nitakushirikisha baadhi tu ya mbinu zinazotumika kupata pesa, na pia mambo muhimu unayopaswa kuyazingatia ili kufanikisha hilo.
Wengi wakiniuliza swali hili, huwa napata picha kwamba, wanahisi blogu ni kama kitu ambacho ukiwa nacho tu chenyewe kinafanya kazi hiyo ya kutengeza faida, na wengine hudhani, pengine walipotoshwa kuwa anaweza anzisha blogu na kuanza kupata pesa bila yeye kama mmiliki wa blogu kuweka juhudi zozote zile!, Hapana, tena ukiwa bloga mpya ndio inakuwa ni ngumu zaidi kupata faida, tazama orodha hii ndogo ya mambo ambayo unapaswa kufanya:
  1. Andaa na anzisha blogu yako
  2. Anza kuandaa na kuchapisha maudhui muhimu kwenye blogu yako
  3. Tafuta wasomaji na wafuatiliaji wa blogu yako
  4. Jenga mahusiano na ushiriki na wasomaji wa blogu yako
  5. Weka mifumo mbalimbali ya kupata pesa kupitia blogu yako
 
Unaona?, kupata pesa ni jambo la mwisho kabisa katika hatua hizo, ila kwa sababu ni hatua tano unaona ni kama rahisi sio?, nitazielezea zaidi hizo hatua ili upate kelewa juhudi unazotakiwa kuwekeza.
1. Andaa na anzisha blogu yako
Ndio, ni lazima uwe na blogu, na uwe unaimiliki wewe mwenyewe, inaweza kuwa rahisi kujifunza jinsi ya kuanzisha blogu kwa kusoma bandiko hili. ambalo ndilo limefanya niulizwe mswali mengi sana kuhusu faida.
2. Anza kuandaa na kuchapisha maudhui muhimu kwenye blogu yako
Blogu haina maana yeyote kama haina maudhui, maudhui(Content) ndio kitu pekee kitakacho tofautisha blogu yako na blogu zingine mtandaoni, maudhui ndio yatakayo kupatia wasomaji na wafuatiliaji wakudumu na hata wapya kwenye blogu yako.
Kimsingi hili ndio jambo la muhimu sana kuzingatia, mfano mwandishi wa habari ana nafasi nzuri ya kuwa na mudhui kwa sababu anakua na habari mpya kila mara, namna atakavyoziandaa habari zake na kuzichapisha kwa wakati inampa fursa kutumia blogu kuwafikia watu wengi kwa urahisi zaidi na wengi watapenda kuarifiwa punde tu unapochapisha habari mpya.
Chochote unachotaka kukizungumzia kwenye blogu yako chaweza kuwa ni kinalenga jamii fulani, au kundi fulani mfano watoto, vijana, wazee, wakulima, wanafunzi nakadhalika, jitahidi kiwe ni bora na chenye upekee. Maudhui mazuri na yenye muelekeo chanya yatawafanya wasomaji wako wajihisi kukufahamu na kukuamini sana hivyo kukuwekea mazingira bora zaidi ya kupata pesa baadae kupitia blogu yako.
3. Tafuta wasomaji na wafuatiliaji wa blogu yako
Blogu yako  ni mpya, hakuna mtu anaifahamu na unaamini una maudhui mazuri, sasa weka juhudi ya kuwapata wasomaji na wafuatiliaji, unatakiwa kuitangaza blogu yako. Muhimu hapa ni kujua ni watu gani (type of people) unaotaka wawe wasomaji na wafuatiliaji wa blogu yako. Kwa mfano umeandaa blogu ya mapishi!, ukishafahamu wasomaji wako ni watu wanaojihusisha na mambo ya mapishi basi fuatilia aina hii ya watu inaweza patikana wapi mtandaoni. Andaa orodha fupi yenye vitu kama:
  • Je!, wanafuatilia blogu zipi zingine zinazofanana au tofauti na maudhui ya blogu yako?
  • Wanashiriki kwenye majukwa gani mtandaoni? mfano (JamiiForums)
  • Kuna vipindi vya radio ama tv wanaweza kuwa wafuatilia pia?
  • Wanatumia mitandao ipi ya kijamii? orodhesha walau mitatu mikuu
  • Wanafuatlia watu gani kwenye hiyo mitandao ya kijamii?
 
Kwenye maeneo hayo utakayobainisha wasomaji unaowahitaji wanaweza kuwepo, wanaweza kuwa wanashiriki kwa kuchangia maoni na kulekezana. Hivyo na wewe inafaa uanze kuwa mshiriki wa maeneo hayo pia ili wakufahamu na pengine unaweza kutumia mwanya huo kuwajulisha na kuwakaribisha kuangalia blogu yako.
Muhimu ni kujenga uwepo wako, ufahamu, na kuchangia/kuongeza dhamani, epuka kuonekana kama mkorofi wa mtandaoni (spammy) kana kwamba unalazimisha watu wajue blogu yako tu, lakini wala huchangii mambo ya msingi wala kushauri.
Pia bila ushiriki wako, unaweza kuandaa bajeti ya matangazo na kutangaza blogu yako kwenye maeneo hayo ili ipate kufahamika.
4. Jenga mahusiano na ushiriki na wasomaji wa blogu yako
Kwa kuzingatia hizo hatua hapo juu, utakuwa na blogu nzuri, yenye maudhui sahihi na bila shaka umeanza kupata  wasomaji, sasa unapaswa kujenga mahusioano ya karibu na wasomaji wako ili waendelee kubaki na pia kukuletea wasomaji wapya.
Jibu maswali yao wanayouliza kuhusu mada husika kwa wingi kadri unavyoweza, pia wasiliana na baadhi yao wanapohitaji mawasiliano nawe kwa njia ya barua pepe nakadhalika.
Kushirikiana na wasomaji ni njia nzuri kukuwezesh akuapata pesa kupitia blogu yako.
5. Weka mifumo mbalimbali ya kupata pesa kupitia blogu yako
Sasa, umeshafanya yote yamsingi, lakini kupata pesa bado, na unahitaji kujaribu na kujuhudi njia mbalimbali kupata pesa. Bado safari ya kujifunza inaendelea, kuna njia nyingi sana za kupata pesa, ila hapa nitorodhesha chache ambazo mimi binafsi huwa nawashauri watu kuzitumia, tena ni njia ambazo bloga wengi huzitumia kupata pesa. Tuanze kujifunza njia hizi:
Kupata pesa kupitia matangazo ya CPC au CPM
Hii ni njia kuu ambayo hutumiwa sana na wamiliki blogu kupata pesa kwa kuweka matangazo madogo madogo kwenye kurasa za blogu zao, ziko aina mbili;
  • CPC/PPC – Cost per Click (au Pay Per Click), matanagazo ambayo yanakuwepo kwenye kurasa au pembeni mwa kurasa ya blogu yako yatakuingizia pesa kila msomaji atakapo gonga (click) tangazo hilo.
  • CPM – Cost per 1000 Impressions, yani kadiri tangazo litakavyoonekana mara nyingi katika nyakati tofauti tofauti na wasomaji tofauti tofauti utapata pesa kutoka kwa anayetangaza.
 
Google Adsense ndio mtandao maarufu wa kuchapisha na kupachika matangazo ya namna hii kwa wamiliki wa tovuti na blogu mbali mbali duniani, na inawalipa wamiliki wa blogu hizi vizuri kadiri blogu husika invyofaya vizuri kuzingatia hatua tulizojifunza awali, matangazo yanayopachikwa huteuliwa kielectroniki kuendana na maudhui, pia lugha ya blogu yako.
Uza matangazo binafsi
Ukiwa na watembeali wengi wa blogu yako kwa siku, sio lazima kutumia mitandao ya matangazo kama Google Adsense, Badala yake Makampuni yanaweza kukufuata moja kwa moja kutaka uwatangazie biashara zao. Unaweza pia kuwasiliana na wahusika moja kwa moja, na kwa kuwa hakuna mtu wa kati, hii inakuwezesha kuweka viwango unvyotaka kutoza kwa kila tangazo na ukapata faida kubwa zaidi.
Tangazo linaweza kuwa mfumo wa picha, video, an au hata chapisho zima kuhusu bidhaa fulani, nakadhalika.
Uza bidhaa za kidigitali
Ikiwa hutaki kuhangaika kutangazia watu wengine, unaweza kutumia blogu yako kutangaza na kuuza bidhaa za kidigitali mfano vitabu, picha, muziki, video n.k.
Unachotakwa kuzingatia hapa, bidhaa utakazoziuza ziandane na maudhui ya blogu yako na pia mahitaji ya wasomaji wako, hutakiwi kuacha kuandika mambo muhimu kwenye blogu yako na kufanya biashara tu, kumbuka watu wanafungu ablogu yako kujifunza, hivyo biashara iwe ni jambo la ziada ili wasomaji wako wasichukizwe na waendelee kufurahia blogu yako.
Andaa unachama wa kulipia kwenye blogu yako
Unaweza kuwa mbunifu zaidi na ukaandaa uanachama wa wasomaji wako ambao watajisajili na kulipia ili kupata huduma na maudhui ya kipekee zaidi, mfano mwandishi wa habari anaweza kuwalipisha wasomaji wake kupata habari mahususi zenye kuchambuliwa kwa kina na hata kushuhusia mahojiano aliyoandaa na baadhi ya watu mashuhuri.
Jenga jina na hadhi ya weledi wako
Blogu inaweza kuwa ni njia ya wewe binafsi kuonyesha uwezo na ufanisi ulionao katika fani mbalimbali na hivyo ukapata mialiko ya kufanya mafundisho, ama kupata kazi za kimikataba ambayo utakubaliana na wateja wako wakulipe.
 
Nimatumaini yangu nitakua nimejibu baadhi ya maswali kwenye chapisho hili, tadhali usiache kujifunza na kuuliza kama una swali jingine, nami nitakuwa huru kukujibu bila shaka.
Nitanendelea kushirikisha taarifa muhimu na mbinu mbali mbali zinazohusu TEHAMA kwa ujumla, hivyo shirikisha bandiko hili na mengine mengi ili nipate wasomaji wengi zaidi kama wewe na hatimae kuongeza ufahamu wa mambo haya katika jamii yetu.
Shirikisha:

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am