Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMULIZI NZURI YENYE KUSISIMUA sehemu ya 3

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 3
Uhakika media
Riwaya: SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA.
Mw/Mtunzi: SEID BIN SALIM
SEHEMU YA 03
Ilipoishia......
" nimekuaribia usingizi wako ee, nsamehe mwaya!
" wala, nlishaamka zamani wala usijali kuhusu hilo.
" mapema yote hii.
" yah kuna masomo jana yalinichanganya ndo nlikuwa nayapitia, si unajua asubuhi kunakuwa hakujachanganya masomo yanaingia?.
" yah nalijua hilo, na wenzio vipi hao tayari au bado wameuchapa. Aliongea akiachia tabasam.
" wao bado wamelala.
" Ok poa, nakuomba ofisini kwangu mara moja basi nna maongezi na wewe samahani lakini. Alisema Sophia lucky akashangaa.
Songa nayo......
" ofisini kwako?
" Yah
" um, kuna tatizo lolote?
" Hapana lucky, ni mambo ya kawaida naitaji tuongee.
" ok sawa nakuja. Alijibu akiwa na wasi wasi wa kuhisi uenda jamaa zake washapeleka malalamiko, Sophia alimuaga na kumuitaji asichelewe kisha akaondoka, lucky alirudishia mlango akasimama katikati mwa mlango na kuangalia vitanda walivyokuwa wamelala wenzake, alitembea taratibu mpaka bafuni ambako alitoa khanga yake na kubaki mtupu, aliachia maji akavuta sabuni, alitengeneza nywele zake zisije kuingia maji, alianza kujimwagia kidogo kidogo huku akilini akijiuliza maswali mengi ambayo hakuwa na majibu yake.
Alimaliza kuoga baada ya kutumia dakika tano hadi sita akiwa bafuni, alivaa nguo haraka haraka akatoka kuelekea ofisini kwa Sophia, akiwa njiani cm yake ilianza kuita, kuangalia kwenye screen alikutana na jina la baba yake, badala ya kupokea na kuwa na furaha kama wanafunzi wengi wa hostel wanapokuwa wanapata bahati ya kupokea cm toka nyumbani, aliikata na kuzima moja kwa moja sura yake nayo ikibadilika kutoka katika mwonekano wa kawaida hadi mwonekano wa chuki.
Alifika kwenye chumba cha Sophia akapita hadi ndani, Sophia aliacha kazi zake alizokuwa anazifanya ili aweze kuongea nae.
" karibu sana lucky.
" asante nshakaribia
" nimemaliza kupata kifungua kinywa umechelewa.
" wala usijali kuhusu hilo.
" Uhm mpenzi!, nimeletewa malalamiko hapa na wenzako, kuwa unavyoishi ni tofauti na wao kabisa kwa nini?. Aliuliza Sophia.
" nlijua tu unaniitia hilo mumy, kiufupi hayo ndo maisha yangu nliyoyachagua kuishi sophia, kila mmoja ana style yake inayomfaa katika maisha, maisha ya chuo nayajua nkianza kujichanganya sitosoma wakati naitaji kufika mbali. ili mradi simtukani mtu, sigombani na mtu, simjibu vibaya mtu, wana haki ya kuishi kivyao na mimi kivyangu, nkiamka nawasalimia, tukinunua chakula tunakula wote wakikosa pesa wakanambia nawapatia. furaha yangu ni kitabu madam mengine siyaitaji. Alisema lucky na kumuacha Sophia njia panda, hakujua ashike wapi aache wapi kwani maelezo yake yalikuwa majibu mazuri tosha, hakuwa na la kuongezea alimwambia amerizika na majibu yake, waliongea mambo mengine huku lucky akimsisitizia kwa kumwambia kuna watu wanapenda kujua binadam wenzao wanaishije ili wawapande kichwani lakini kwake hilo haliwezekani.
Sophia alimruhusu arudi chumbani kwake, dada huyo ni mwanamke aliekuwa na akili nyingi sana za kumtega mtu, kilichokuwa kichwani mwake baada ya kumruusu aondoke alikijua yeye, ila muda waliotumia kuongea na maongezi waliyoyazungumza na jinsi walivyokuwa wanaongea, alipata kufahamu kuna tatizo linamsumbua bidada lucky japo haitaji kulionesha.
" Unaonekana mpole na mtaratibu lucky ila una tatizo linakusumbua na mimi ntalifanyia kazi mpaka nlifahamu.. alisema peke yake.
Lucky alirudi chumbani akawakuta wenzake bado wamelala, aliwaamsha akawakalisha kitako kutaka kujua kitu gani kimewakuta hadi kwenda kwa Sophia kumweleza matatizo yake.
" Friends, nawaeshim na mimi naomba mnieshim, msione kwa kuwa nakaa kimya siongei mkajua ni mjinga na zoba kiiivo tafadhalini, kila mmoja ana maisha yake ya kuishi, na kila mtu hapa amekuja kwa pesa zake na akili zake, hivyo sitaki mniingilie kwenye maisha yangu, nkiwatukana nendeni mkaseme, lakini ili hali siwatukani siwadharau tafadhali tueshimiane, kama hamuitaji kuishi na mimi semeni na kama mnahisi nawanyima uhuru waambieni wawapatie chumba kingine mniache peke yangu kwa sababu uwezo wa kulipa chumba kizima hiki nnao, msitake kunipanda kichwani nawaombeni na nawaombeni tena, maisha yangu hamyajui niacheni kama nlivyo. Alisema kwa hasira.
" lakini lucky!, kitu gani sisi hapo tumekosea?. Tunaumia tunapoona unaishi kiunyonge mpenzi, usituchukulie vibaya unajiathiri kisaikolojia lucky. Alisema maryam.
" siitaji niacheni niaribike kisaikolojia, naishi nitakavyo na sii mtakavyo Hey!, kwani lazima?. Alisema lucky.
" Basi dada yaishe, tusamehe kwa kirehe rehe chetu cha kutoa kwaito zetu hapa hadi kwa Sophia. Alisema tunu.
" ila na sisi umbea umetuzidi una haki ya kutuchamba. Alidakia Amina.
Tunu na amina walisimama wakavaa nguo zao na kutoka nje wakiwa wamepandwa na hasira kwenda kumwangalia mhudumu ambae huwa anawapatia chai, walimtaka maryam avae waende ila akagoma, walitoka chumbani akabaki maryam na lucky, maryam alikuwa ana huruma sana alijisikia vibaya namna mwenzake alivyo lalamika, hakutaka amuaminishe kuwa yeye ni mbaya wake.
" lucky, sijafunzwa kumuacha mtu anaelia akiendelea kumwaga machozi yake na mimi kutoka nje, maneno yako yanaonesha kiasi gani umekasirika juu ya maamuzi yetu, tokea uingie humu sijawai kukuona ukiongea hivyo, naomba unisamehe sana kwa kufanya kitu ambacho hujaridhia, nisamehe mimi na wenzangu, siko happy kiukweli kukuona ukiuzunika japo itanilazimu sasa. alisema maryam.
" Hivi unajua huyu dem simwelewi Amina ee!. Baada ya kuwa wako nje Tunu alisema kumwambia mwenzake.
" hata mimi, eti nna uwezo wa kuchukua room nzima peke yangu msiniingilie, Haa!, huyu wakuja nini.
" linavyoongea sasa kama mdomo umemeza flash, yani hata yale mapozi hana.
" kaniharibia siku asubuhi asubuhi Akyamungu, sijui mudi kama ntamkuta aniletee bia nipoze akili kwanza. Alisema amina akipeleka mkono kichwani kukuna nywele zake zilizokuwa tim tim flan.
" tena sio moja, huyu mtoto mimi nataka nimchangamkie nimkorogee Kiswahili ajione kama kunya, eti hooo mna maisha yenu na mimi nna maisha yangu yani kaniboaaa. Alisema tunu.
" ila kirehe rehe chetu na sisi, ashuo gani hadi midomo ikatupwaya kwenda kusema?.
" kirehe rehe kihere here mwenzangu na nimekoma kuingilia maisha ya watu yasiyonihusu. Alisema tunu. walifika chini walikokuwa wanapatikana wahudumu wakamuona mudi waliemzoea, walimpatia maagizo ya nini awapalekee kisha wakageuza kurudi.
Maryam ndani aliendelea kumuomba msamaha lucky ili amsamehe kwa kumfanya akose raha baada ya kuchukuana na wenzake na kwenda kwa sofia, lucky alimwelewa akamwambia asijali ni mambo ya kawaida.
" Ok my friend, napenda kuiona furaha ya mtu, sipendi kuipoteza maana najua siwezi kuilipa. Nambie ungependa kula nini morning hii!. Alisema maryam mara alipoona tabasam la lucky, aliinuka kitandani akaweka mkono kwenye mfuko wa nguo yake iliyokuwa umetundikwa kwenye henga kuangalia kama kuna pesa.
" Sijisikii hata kula kitu mumy usijali.
" No Lucky, asubuhi lazima kuwepo na kifungua kinywa, kama umenisamehe naomba unambie utakula nini!. Alisema akiachia tabasam, mkononi tayari alishikilia shiling elfu 10 ya kitanzania.
" Unataka kwenda kuagiza?. Aliuliza lucky
" Yes.
" Poa, nchukulie soseji mbili, chai ya maziwa juis na chapati moja.
" Ok poa.
Alitoka maryam kwenda kuchukua chai, alipofungua mlango akakutana na wakina Amina wao wakirudi.
" ulikuwa bado unaongea na huyo mtu?. Tunu alimuuliza.
" yah nlikuwa naongea nae.
" ana jipya gani.
" katusamehe.
" kwani tumemkosea.
" Tunu acha hizo bhana, huoni kama tumemkosea kwenda kwa sofia bila kumwambia?.
" Duh!. Tunu alitoa macho ya mshangao.
" Ujue tunu huyu nae ndo wale wale huruma huruma. Alidakia Amina.
" sio huruma huruma, ili hali hatutukani, tukimsalimia anajibu vizuri, kwa nini tumuingilie katika maisha yake?. Tumuache kama alivyo. Alisema maryam.
walipomuangalia maneno yake wakajua tayari yupo kwa ajili ya kumtetea lucky, walimruhusu aendelee na safari yake ya aendako nao wakaendelea kuwepo nje kupiga umbea kabla ya kuingia ndani.
" Kashakuwa rafiki yake huyu. Alisema amina.
" Muache akizingua na yeye si tunamsheet tu.
" Anajifanya huruma huruma, wee lini paka na mbwa wakakaa pamoja bila kukoromeana?. Jitu liko kama zombie halijua kuongea, muda wote kuvimbisha mashavu tu kama kabugia pili pili urafiki nae wa nini?.
" ndo hapo sasa!, hata mi nashangaa.
Walimaliza kuongea wakaingia ndani na kumkuta lucky yuko kitandani amelala, tayari alikuwa kwenye mkusanyiko wa mawazo, machozi yalikuwa yanamtiririka upande upande, walimuangalia hawakuitaji kumshtua, kila mmoja alipanda kitandani kwake akachukua cm na kuanza kuchart, waliweka phoni maskioni wakawa hawana habari wasijue kinachoendelea, lucky alikuwa katika wakati mgumu sana, hakuacha kukumbuka baadhi ya mambo yaliyomtokea nyumba ambayo yalisababisha mara kadhaa kumfanya akose raha na kuachia kilio cha bila kutaka wala kutaraji.
Maryam alirudi baada ya kuagiza vya kuagiza, akiwa mlangoni aliwaangalia amina na tunu akaona ambavyo hawana habari na mtu wako bize na kusikiliza miziki, alipomuangalia lucky akajua tayari hayuko sawa, alitikisa kichwa chake kumsikitikia, ni yeye pekee alibakia kumuonea huruma, alisogea akakaa pembeni ya alikolala.
" Lucky. Alimuita kwa sauti ya taratibu, lucky alishtuka akafuta machozi yaliyokuwa yanatoka.
" Usijaribu kufuta chozi la kinyonge wakati haiwezekani. Mbona unajaribu kuficha maradhi ya kidonda cha nje ya mwili wakati kila mmoja anakiona?. Sii vizuri lucky unavyofanya, hali yako hainiusu lakini naumia kuona wenzio tunafurahi wewe huna furaha. Alisema maryam katika hali ya huzuni baada ya kuona lucky anafuta machozi, lucky maneno aliyoambiwa na binti huyo yalimuingia akilini, aliinuka akakaa na kumshika pajani.


NINI KITAENDELEA KATIKA EPISODE YA NNE 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am