Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali

Report ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali


RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2016/17, imegusa mambo makubwa saba, ikiwemo udhibiti mkubwa na matumizi mazuri ya fedha za umma.


Kwa mujibu wa CAG, ofisi yake imetoa hati 561 ambapo hati 502 sawa na asilimia 90 zinaridhisha, hati 45 sawa na asilimia 8 zina mashaka, hati 7 sawa na asilimia 1 haziridhishi na hati 7 sawa na asilimia 1 ni mbaya.

Ripoti hiyo pia imebainisha kutolewa kwa hati chafu kwa baadhi ya halmashauri, utendaji mzuri wa Serikali Kuu na Deni la Taifa.

Maeneo mengine ni mamlaka za serikali za mitaa, utendaji wa mashirika ya umma, miradi ya maendeleo na ukaguzi maalumu.

Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Juma Assad alimkabidhi Rais John Magufuli vitabu 6 vya ripoti hiyo, Ikulu, Dar es Salaam jana.

Ripoti hizo ni pamoja na ripoti ya Serikali Kuu, ripoti ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, ripoti ya Mashirika ya Umma, ripoti ya miradi ya maendeleo, ripoti ya Ukaguzi na Ufanisi na ripoti 10 zinazohusu ukaguzi wa ufanisi katika sekta mbalimbali.

Profesa Assad alisema serikali imeendelea kufanya vizuri, kwani kumekuwa na hatua nzuri ya kuongeza hati zinazoridhisha na kupunguza hati za mashaka na mbaya.

Alibainisha kuwa mashirika ya umma, yamepata hati safi kwa asilimia 96, Mamlaka ya Serikali za Mitaa asilimia 90 na Serikali Kuu imepata asilimia 86 kwa sababu ndani yake kuna vyama saba vya siasa ambavyo hakukuwa na makubaliano juu ya hesabu zake.

Baadhi ya vyama hivyo, kwa mujibu wa CAG, ni Tanzania Labour Party (TLP), Alliance for Tanzania Democratic Change, Demokrasia Makini na Chama cha Sauti ya Umma. Alisema sheria inamtaka kuvikagua vyama vyote vya siasa bila kujali kama vinapata ruzuku au la.

Serikali za Mitaa Baadhi ya halmashauri zilipata hati chafu. Halmashauri hizo ni Kigoma-Ujiji, Kigoma Vijijini na Pangani. Baada ya taarifa hiyo ya CAG, Rais Magufuli alimwagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo kuwasimamisha kazi wakurugenzi wa halmashauri hizo tatu kutokana na halmashauri zao kupata hati chafu.

Serikali Kuu Kwa mujibu wa Profesa Assad, kwa upande wa Serikali Kuu, kati ya taasisi 217 zilizokaguliwa, taasisi 204 zilipata hati safi ambayo ni sawa na asilimia 86; taasisi 22 ambazo ni sawa na asilimia tisa zimepata hati zenye shaka, wakati asilimia mbili ya taasisi hizo zikipata hati zisizoridhisha.

Aidha, katika eneo hilo pia, Prof Assad alisema kuwa kuna kesi za rufaa ya kodi zenye thamani ya Sh trilioni 4.4 ambazo mpaka sasa bado hazijafanyiwa uamuzi na Mahakama, wakati pingamizi za kodi zikigharimu Sh bilioni 739.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, Rais Magufuli alimuagiza Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango kujadiliana na Jaji Mkuu ili kesi hizo ziamuliwe haraka.

Kwa mujibu wa CAG, walibaini kuwepo kwa mitambo ya kuchenjulia madini mkoani Mwanza, Shinyanga na wilayani Kahama kufanya kazi bila ya kuwa na leseni, hivyo kuingiza hasara ya Sh bilioni 232. Deni la Taifa Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, deni la Taifa limeongezeka kutoka Sh trilioni 41 mwaka uliopita hadi kufikia Sh trilioni 46 sasa.

Alisema kuwa kuna ongezeko la shilingi trilioni tano ambazo ni sawa na asilimia 12.

Mamlaka za serikali za mitaa Katika eneo hilo, CAG alisema kuwa Serikali za Mitaa 146 hazikupata Sh bilioni 582 kama sehemu ya bajeti ya maendeleo ya Serikali za Mitaa.

Aliongeza kuwa Sh bilioni 532 sawa na asilimia 51 ya fedha maendeleo, pia hazikupelekwa kweye serikali za mitaa 167. “Lakini pia fedha za miradi ya ndani kwenye Serikali za Mitaa hazikukusanywa aidha kwa kuwatumia mawakala au halmashauri zenyewe.

Serikali za Mitaa 140 hazikukusanya Sh bilioni 116 sawa na asilimia 22 ya mapato yake. Pia Profesa Assad alieleza kuwa vitabu 379 vya mapato hakuviona, hivyo hajui ni kiasi gani cha mapato kimepotea, lakini pia miradi mitatu yenye thamani ya Sh bilioni 1.6 kwenye Halmashauri za Biharamulo, Karagwe na Mpwapwa, imechelewa kukamilishwa.

Udhai

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya...

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza...

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Siga...

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni...

SIMULIZI NZURI NA YA KUSISIMUA sehemu ya 2

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 2 uhakika media Riwaya: SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA. Mtunzi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA PILI Ilipoishia... " hhhhhmmmmm. Aliguna tunu, kumbe na wewe umo?. Walinyanyuka na kicheko kila mmoja akabeba mkoba wake na kwenda darasani. lacky alitoka bafuni akiwa na khanga moja mwilini akakaa kitandani na kujifuta futa maji, hakukaa dakika akanyanyuka na kusogea kwenye kioo kujiangalia mwili wake wote ulivyo. Alivuta mafuta aina ya lotion akajipaka baadhi ya sehemu za mwili wake, alipomaliza aliitoa khanga mwili ukabaki utupu kisha akavaa nguo za ndani zilizokuwa kwenye henga.. Alimaliza kwa nguo za chuo akabeba mkoba na kutoka ndani, hadi anafika darasan hakuna alieweza kumpa hi kwa sababu ya kusikojulikana sana na watu, kwa alivyokuwa anajiweka hakuna aliweza kumzoea kwani hata mbinu ya kumuingia haikuwepo, wapo wanaume waliojifanya midomo mirefu kutaka kuingiza mistari ya kumtongoza kutokana na uzuri wa mvuto al...

SIMULIZI NZURI YENYE KUSISIMUA sehemu ya 3

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 3 Uhakika media Riwaya: SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA. Mw/Mtunzi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA 03 Ilipoishia...... " nimekuaribia usingizi wako ee, nsamehe mwaya! " wala, nlishaamka zamani wala usijali kuhusu hilo. " mapema yote hii. " yah kuna masomo jana yalinichanganya ndo nlikuwa nayapitia, si unajua asubuhi kunakuwa hakujachanganya masomo yanaingia?. " yah nalijua hilo, na wenzio vipi hao tayari au bado wameuchapa. Aliongea akiachia tabasam. " wao bado wamelala. " Ok poa, nakuomba ofisini kwangu mara moja basi nna maongezi na wewe samahani lakini. Alisema Sophia lucky akashangaa. Songa nayo...... " ofisini kwako? " Yah " um, kuna tatizo lolote? " Hapana lucky, ni mambo ya kawaida naitaji tuongee. " ok sawa nakuja. Alijibu akiwa na wasi wasi wa kuhisi uenda jamaa zake washapeleka malalamiko, Sophia alimuaga na kumuitaji asichelewe kisha akaondoka, l...

Hii ndio barua ya prof: Kitila Mkumbo kwenda kwa mkuu wa kanisa la KKKT

Hii ndio Barua ya Profesa Kitila Mkumbo Kwenda kwa Mkuu wa Kanisa la KKKT Uhakika media 5  · 1 hour ago Baba Askofu Dkt. Fredrick Shoo, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) S. L. P. 3033 ARUSHA. Mheshimiwa Baba Askofu, Shalom!  YAH: MAMBO MATANO AMBAYO HAYAPONYI KATIKA WARAKA WA MAASKOFU WA KKKT   Jina langu ni Kitila Mkumbo, muumini katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), ambalo wewe ndiye mkuu wake. Kikazi, mimi ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Dodoma. Kitaaluma, mimi ni mhadhiri mwandamizi katika Saikolojia na Elimu nikiwa na cheo cha Profesa mshiriki katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.  Mheshimiwa Baba Askofu, kwa unyenyekevu mkubwa nimeamua kukuandika barua hii ili kutoa maoni yangu binafsi kwa kanisa unaloliongoza kupitia kwako kuhusu maudhui ya waraka uliotolewa na waheshimiwa maaskofu wa KKKT siku ya Jumamosi tarehe 24 Machi 2018. Waraka huo ulitarajiwa kusomwa katika makanisa siku ya Jumapili...

Misingi bora ya ufugaji wa mbuzi kibiashara

Misingi Bora Ya Ufugaji Wa Mbuzi Kibiashara Uhakika media · 20 minutes ago NAMNA BORA YA UFUGAJI.   1. Wafugwe kwenye banda bora.   2. Chagua kulingana na sifa zao na lengo la ufugaji (uzalishaji) nyama au maziwa.   3. Walishwe chakula sahihi kulingana na umri.   4. Kuzingatia ushauri wa mtaalamu wa mifugo hasahasa namna ya udhibiti wa magonjwa.   5. Kuweka kumbukumbu za uzalishaji.   6. Kuzalisha nyama au maziwa bora yanaokidhi mahitaji ya soko.   SIFA ZA ZIZI AU BANDA BORA LA MBUZI.   1. Banda bora linatakiwa liwe ni lenye kuweza kuwakinga mbuzi au kondoo na mashambulizi ya wanyama wakali (hatari) na wezi.   2. Liwepo sehemu ambayo maji hayawezi kutuama.   3. Mabanda yatenganishwe kulingana na umri.   4. Liwe na ukubwa ambao linaweza kufanyiwa usafi.   Kama utafuga mbuzi kwa kuwafungia (shadidi) muda wote zingatia yafuatayo:-   1. Banda imara lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya,upepo/mvua.   2. Lenye hewa ya...

Idara ya uhamiaji wafunguka kuhusu uraia wa Kidao

Idara ya Uhamiaji yafunguka kuhusiana na uraia wa Kidao Uhakika media 2  · 58 minutes ago Idara ya Uhamiaji nchini imesema inaendelea na uchunguzi juu ya uraia wa Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Wilfred Kidao.  Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara hiyo, Ally Mtanda, amesema bado wapo kwenye uchunguzi na pale utakapokamilika watakuwa na majibu sahihi ya kusema.  "Bado tunaendelea na uchunguzi kuhusiana na suala hilo, pale utakapokamilika tutakuja na majibu sahihi ya kusema, kwa sasa bado haujakamilika" alisema Mtanda.  Hatua hiyo ilikuja mara baada ya kuelezwa kuwa Kaimu Katibu Mkuu huyo hana uraia wa Tanzania.