RIWAYA NA HADITHI ZA KUSISIMUA
Mtuhumiwa 03
Posted by uhakika media
Eh! Kunyongwa tena? Huyu jamaa ni nani kwani?
Binti alizidisha idadi ya viulizo akilini mwake dhidi ya yule jamaa.
“Sasa we’ jitie kiburi halafu uone jinsi kitanzi kinavyounyofoa uhai wako mbovu kutoka mwilini mwako, bwege wewe!” Sajenti alimalizia kumkoromea yule jamaa, kisha akausukuma chini kwa nguvu uso wa yule jamaa na kumpigiza sakafuni kisogo chake. Maumivu makali yalimpata kichwani kwani jamaa alifumba macho kwa uchungu na akashika kichwa chake kwa mikono yake yote miwili, akigaragara huku akiinua juu magoti yake akiwa amelalia mgongo pale sakafuni.
“Ai jamaani…Looh!” Alisikitika kwa simanzi yule msichana.
“Koplo!” Sajenti aliita kwa sauti.
“Afande!”
“Piga simu kwa huyo mjomba’ake aje amchukue huyu mgeni wake hapa…upesi!”
“Yes, Sir!”
Kisha yule Sajenti alimgeukia tena yule jamaa, ambaye sasa alikuwa amekaa chini huku ameegemea ukuta akikohoa huku akitikisa kichwa kwa uchungu na masikitiko. Alimwinamia pale chini na kumtomasa kwa nguvu kifuani kwa kidole chake cha shahada.
“Nakupa nafasi ya mwisho bwana mdogo. Sasa ni saa sita na nusu usiku. Nitakulaza hapa kituoni. Asubuhi nakupatia escort ya kuhakikisha kuwa unatoka nje ya mkoa huu…sasa ole wako urudi tena…utajuta kuzaliwa!”
Baada ya hapo jamaa alibebwa juu juu na kutupwa kwenye chumba cha mahabusu.
Yule binti alibaki akitazama hali ile kwa huzuni kubwa. Alitamani amwambie neno lolote la kumliwaza yule jamaa lakini hakulipata neno wala nafasi ya kufanya hivyo.
Muda wote wakati haya yanatokea, yule jamaa wala hakuwa na habari na yeye. Ni kama kwamba yule binti hakuwepo kabisa katika eneo lile.
2
Jaka ndilo jina la yule jamaa.
Jaka Brown Madega ndio jina lake kamili.
Jioni hii alikuwa amejiinamia nje ya nyumba moja ndogo iliyojengwa kwa tope na kuezekwa kwa bati kama jinsi nyumba nyingi nyingine katika eneo lile zilivyokuwa. Kwa mbali aliweza kusikia muziki wa zamani wa kikongo kutoka kwenye moja kati ya vilabu vingi vya pombe za kienyeji vilivyotawala eneo lile.
Nyumba aliyokuwa amekaa yeye ilikuwa ni ya vyumba viwili na sebule ndogo iliyotawaliwa na vigoda vya kigogo na majamvi. Jiko lilikuwa nyuma ya nyumba hiyo ambako pia ndipo kilipokuwa choo cha shimo, mlango wake ukiwa ni kipande cha gunia. Bafu lilikuwa kando ya choo. Kuta nne ambazo juu hazikuezekwa kitu chochote na uwazi ulioachwa kwenye moja ya kuta zile nne kuwa kama mlango ukiwa umefunikwa kwa kipande cha gunia kwa ajili ya ile faragha ya kibinaadamu pindi muogaji atakapohitaji faragha.
Mbele ya nyumba ile kulijengwa ukuta mdogo wa kozi zipatazo nne hivi kwa kutumia vipande vya matofali ya kuchoma. Ukuta huu ulitokea kwenye kona ya kulia ya nyumba ile na kwenda mbele kama hatua kumi na tano hivi za mtu mzima, kisha ukarudi kuelekea kushoto na kuacha uwazi mdogo usawa wa mlango wa mbele wa nyumba ile, halafu ukaendelea na kukutana na ukuta mwingine uliotokea kona ya kushoto ya nyumba ile.
Ni juu ya ukuta uliotokea kona ya kushoto ya nyumba hii ambapo huyu mtu aitwaye Jaka Brown Madega alikuwa amejiinamia, mgongo wake akiwa ameuegemeza kwenye ukuta wa sebule ya nyumba ile, miguu yake akiwa ameikunja kwa mbele, paji lake la uso akiwa ameliegemeza juu ya magoti yake hali akiwa amekumbatia miguu yake kwa kuzungusha mikono yake chini kidogo ya magoti yake. Alionekana kuwa ni mwenye mawazo mazito.
Ni siku nne sasa zimepita tangu alipopambana na ule mkasa uliotokea katika usiku wa mvua nzito ndani ya jiji la Dar es Salaam.
Baada ya kulala pale kituoni usiku ule, asubuhi na mapema kabla hata mkuu wa kituo kile hajaingia, yule Sajenti aliyekuwa akiongoza ile doria iliyomkumba usiku ule, ambaye Jaka alimjua kama Sajenti John Vata, alimtoa mahabusu na kumpakia ndani ya ile ile Land Rover iliyowabeba usiku uliopita na kuelekea naye mjini. Safari hii aliyekaa katikati ya Sajenti John Vata na dereva alikuwa ni Jaka. Nyuma ya ile Land Rover alikuwako Koplo mmoja mnene mwenye sura ya kibwege sana ambaye alikuwa na bunduki aina ya SMG aliyoipakata mapajani mwake.
“S’jui kwa ni’ n’sikur
Mtuhumiwa 03
Posted by uhakika media
Eh! Kunyongwa tena? Huyu jamaa ni nani kwani?
Binti alizidisha idadi ya viulizo akilini mwake dhidi ya yule jamaa.
“Sasa we’ jitie kiburi halafu uone jinsi kitanzi kinavyounyofoa uhai wako mbovu kutoka mwilini mwako, bwege wewe!” Sajenti alimalizia kumkoromea yule jamaa, kisha akausukuma chini kwa nguvu uso wa yule jamaa na kumpigiza sakafuni kisogo chake. Maumivu makali yalimpata kichwani kwani jamaa alifumba macho kwa uchungu na akashika kichwa chake kwa mikono yake yote miwili, akigaragara huku akiinua juu magoti yake akiwa amelalia mgongo pale sakafuni.
“Ai jamaani…Looh!” Alisikitika kwa simanzi yule msichana.
“Koplo!” Sajenti aliita kwa sauti.
“Afande!”
“Piga simu kwa huyo mjomba’ake aje amchukue huyu mgeni wake hapa…upesi!”
“Yes, Sir!”
Kisha yule Sajenti alimgeukia tena yule jamaa, ambaye sasa alikuwa amekaa chini huku ameegemea ukuta akikohoa huku akitikisa kichwa kwa uchungu na masikitiko. Alimwinamia pale chini na kumtomasa kwa nguvu kifuani kwa kidole chake cha shahada.
“Nakupa nafasi ya mwisho bwana mdogo. Sasa ni saa sita na nusu usiku. Nitakulaza hapa kituoni. Asubuhi nakupatia escort ya kuhakikisha kuwa unatoka nje ya mkoa huu…sasa ole wako urudi tena…utajuta kuzaliwa!”
Baada ya hapo jamaa alibebwa juu juu na kutupwa kwenye chumba cha mahabusu.
Yule binti alibaki akitazama hali ile kwa huzuni kubwa. Alitamani amwambie neno lolote la kumliwaza yule jamaa lakini hakulipata neno wala nafasi ya kufanya hivyo.
Muda wote wakati haya yanatokea, yule jamaa wala hakuwa na habari na yeye. Ni kama kwamba yule binti hakuwepo kabisa katika eneo lile.
2
Jaka ndilo jina la yule jamaa.
Jaka Brown Madega ndio jina lake kamili.
Jioni hii alikuwa amejiinamia nje ya nyumba moja ndogo iliyojengwa kwa tope na kuezekwa kwa bati kama jinsi nyumba nyingi nyingine katika eneo lile zilivyokuwa. Kwa mbali aliweza kusikia muziki wa zamani wa kikongo kutoka kwenye moja kati ya vilabu vingi vya pombe za kienyeji vilivyotawala eneo lile.
Nyumba aliyokuwa amekaa yeye ilikuwa ni ya vyumba viwili na sebule ndogo iliyotawaliwa na vigoda vya kigogo na majamvi. Jiko lilikuwa nyuma ya nyumba hiyo ambako pia ndipo kilipokuwa choo cha shimo, mlango wake ukiwa ni kipande cha gunia. Bafu lilikuwa kando ya choo. Kuta nne ambazo juu hazikuezekwa kitu chochote na uwazi ulioachwa kwenye moja ya kuta zile nne kuwa kama mlango ukiwa umefunikwa kwa kipande cha gunia kwa ajili ya ile faragha ya kibinaadamu pindi muogaji atakapohitaji faragha.
Mbele ya nyumba ile kulijengwa ukuta mdogo wa kozi zipatazo nne hivi kwa kutumia vipande vya matofali ya kuchoma. Ukuta huu ulitokea kwenye kona ya kulia ya nyumba ile na kwenda mbele kama hatua kumi na tano hivi za mtu mzima, kisha ukarudi kuelekea kushoto na kuacha uwazi mdogo usawa wa mlango wa mbele wa nyumba ile, halafu ukaendelea na kukutana na ukuta mwingine uliotokea kona ya kushoto ya nyumba ile.
Ni juu ya ukuta uliotokea kona ya kushoto ya nyumba hii ambapo huyu mtu aitwaye Jaka Brown Madega alikuwa amejiinamia, mgongo wake akiwa ameuegemeza kwenye ukuta wa sebule ya nyumba ile, miguu yake akiwa ameikunja kwa mbele, paji lake la uso akiwa ameliegemeza juu ya magoti yake hali akiwa amekumbatia miguu yake kwa kuzungusha mikono yake chini kidogo ya magoti yake. Alionekana kuwa ni mwenye mawazo mazito.
Ni siku nne sasa zimepita tangu alipopambana na ule mkasa uliotokea katika usiku wa mvua nzito ndani ya jiji la Dar es Salaam.
Baada ya kulala pale kituoni usiku ule, asubuhi na mapema kabla hata mkuu wa kituo kile hajaingia, yule Sajenti aliyekuwa akiongoza ile doria iliyomkumba usiku ule, ambaye Jaka alimjua kama Sajenti John Vata, alimtoa mahabusu na kumpakia ndani ya ile ile Land Rover iliyowabeba usiku uliopita na kuelekea naye mjini. Safari hii aliyekaa katikati ya Sajenti John Vata na dereva alikuwa ni Jaka. Nyuma ya ile Land Rover alikuwako Koplo mmoja mnene mwenye sura ya kibwege sana ambaye alikuwa na bunduki aina ya SMG aliyoipakata mapajani mwake.
“S’jui kwa ni’ n’sikur
Maoni
Chapisha Maoni