Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MBINU 11 ZA KUPUNGUZA UZITO NA UNENE BILA KUFANYA MAZOEZI WALA KUFUNGA KULA

MBINU 11 ZA KUPUNGUZA UZITO NA UNENE BILA MAZOEZI WALA KUFUNGA KULA
Kuendelea kutegemea mazoezi au kufunga kula au kupunguza kula kunaweza kusiwe msaada kwa baadhi ya wengine wanaotaka kupunguza uzito na unene wa miili yao.
Hata hivyo zipo mbinu chache unazoweza kuzitumia na ukaweza kudhibiti uzito wako.
Bila kukupigisha stori nyingi hapa chini nakuelezea mbinu hizo bila kuchelewa kama ifuatavyo:
Mbinu 11 za kupunguza uzito na unene bila mazoezi wala kufunga kula
1. Kula chakula pole pole
Ubongo wako unahitaji muda wa kutosha kushughulika na hilo tendo la kutafuna na kumeza chakula.
Kula pole pole kunahusiana moja kwa moja na kuweza kula chakula kichache na kujisikia kushiba.
Ni muda gani unatumia kumaliza chakula chako unaweza kuathiri pia uzito wako.
Utafiti unaonyesha watu wanaokula kwa haraka haraka hutokewa kuwa na uzito mkubwa pia ukilinganisha na wale wanaokula pole pole.
Jaribu hii haitakugharimu kitu.
2. Tumia sahani ndogo kwa vyakula visivyo na afya
Kama itakutokea ukataka kula vyakula visivyo na afya ambavyo huongeza uzito kirahisi basi jaribu kutumia sahani ndogo na siyo unayotumia kila siku. Mara nyingi watu wengi chakula kinapoisha kwenye sahani hujiona tayari inatosha.
Hivyo sahani ndogo inakifanya chakula kionekane kingi na kikubwa na hivyo kuridhisha macho na njaa yako kwa ujumla.
Kazi inabaki kuwa kwako mara zote.
3. Kula zaidi protini
Vyakula vyenye protini vina matokeo makubwa upande wa njaa. Vyakula hivi vinakufanya ujisikie umeshiba kwa kipindi kirefu kama ilivyo kwa vyakula vyenye nyuzinyuzi.
Kama kwa sasa asubuhi unakula chakula cha asubuhi chenye wanga mwingi kama mikate, chapati au maandazi au hata wali basi unaweza kuhamia kula vyakula vyenye protini nyingi kama vile mayai.
Vyakula vingine vyenye protini nyingi ni pamoja na korosho, samaki, mtindi, parachichi, karanga, mbegu za maboga, nk nk
4. Weka mbali vyakula visivyo na afya
Vyakula vile unavyofahamu kwa hakika kwamba huongeza uzito na unene kirahisi ni vema ukavihifadhi mbali na macho yako hivyo hutashawishika kutaka kuvila.
Hili nalo ni rahisi kulitekeleza na kazi inaendelea kuwa kwako tu.
5. Kula zaidi vyakula vyenye nyuzinyuzi
Vyakula vyenye nyuzinyuzi (faiba) vinao uwezo wa kukufanya ujisikie umeshiba kwa muda mrefu.
Vyakula hivi mara nyingi hutokana na mimea hasa maharage, machungwa, parachichi, mbegu za maboga, karoti, mayai, ndizi, nk
6. Acha kukaa kwenye kiti masaa mengi
Umewahi kujaribu kufanya mazoezi, kubadili chakula au hata kufunga na bado ukawa unasumbuliwa na kitambi au uzito kuwa mkubwa? Basi jibu la tatizo lako ni kukaa kwenye kiti masaa mengi.
Utafiti unaonyesha kukaa tu kwenye kiti hata kama hauli chakula kingi bado utaendelea kuongezeka uzito.
Kwahiyo kama unataka kuondoa kitambi au tumbo au kupungua uzito kwa haraka acha kukaa masaa mengi kwenye kiti, hata kama kazi yako ni ya ofisini jaribu namna unaweza kupata meza ya kusimama huku unaendelea na kazi yako.
7. Pakuwa vyakula visivyo na afya kwenye sahani nyekundu
Mbinu hii ya kushangaza ni kuwa unachohitaji kufanya ni kuweka chakula ambacho si afya yaani vile vinavyoongeza uzito kama chipsi, maandazi na vingine kama hivyo katika sahani ambayo ni nyekundu .
Utafiti mmoja ulionyesha kuwa watu walifanikiwa kula chakula kidogo baada ya kuwa wanawekewa chakula kwenye sahani nyekundu ukilinganisha na wakati walipowekewa kwenye sahani za rangi nyingine.
Maelezo ni kuwa mara nyingi tunahusianisha rangi nyekundu na alama ya kusimama na maonyo mengine katika maisha yetu ya kila siku.
8. Acha vinywaji vyenye sukari sana
Viongeza utamu vya kutengenezwa (artificial sweetners) na sukari kwa ujumla vimekuwa vikiwekwa kwenye vinywaji vingi miaka ya sasa.
Vinywaji vyenye sukari kama soda vimekuwa vikihusishwa na kuongezeka kwa mwili moja kwa moja.
Ni rahisi zaidi kuongezeka uzito ukitumia vinywaji hivi kwakuwa nishati yake ni rahisi kubebeka na kuvumilika tofauti na ile ya kwenye vyakula vigumu.
Kukaa mbali na vinywaji hivi na juisi nyingine zozote za dukani na hata za nyumbani zenye sukari ni namna nzuri ya kudhibiti uzito bila kuhitaji mazoezi wala kufunga kula.
Badala yake kunywa zaidi zaidi maji au chai ya kijani (green tea) au chai ya viungo mbalimbali (spiced tea) ukitumia asali kwa mbali badala ya sukari.
9. Pata usingizi mzuri na epuka msongo wa mawazo
Linapokuja suala la kuwa na afya bora kupata usingizi mzuri na kutokuwa na msongo wa mawazo (stress) ni vitu viwili haviepukwi. Usingizi na sress vyote viwili vinaweza kuwa na matokeo ya moja kwa moja kuhusu njaa na uzito wako.
Ukosefu wa usingizi mzuri kunaweza kuzisababishia homoni zinazohusika na kuweka sawa njaa (leptin na ghrelin) kutokufanya kazi zake vizuri. Homoni nyingine iitwayo “cortisol” ambayo inahusika na utulivu pia inakuwa imeongezeka sana wakati unapokuwa na msongo wa mawazo.
Homoni hizi zikiwa zimesumbuliwa hivyo kiasi chako cha njaa kitaongezeka pia uhitaji wako wa kula vyakula visivyo na afya utaongezeka mara dufu.
Kile ulikuwa hujuwi ni kuwa kama hupati usingizi mzuri na wa kutosha unakuwa na uwezekano mkubwa wa kupatwa na ugonjwa wa kisukari aina ya pili.
10. Wakati unakula usitumie simu au kompyuta
Kuwa makini na akili yote ukiiweka katika chakula tu kunaweza kusaidia kula kidogo.
Watu ambao wanakula huku wanatumia simu, kompyuta au wanaangalia luninga (TV) au wanacheza gemu huwa wanakula chakula kingi bila wao kujua.
Jaribu mbinu hii kwa miezi kadhaa na uniletee mrejesho, WhatsApp +255769142586
11. Kunywa maji mara kwa mara
Kunywa maji mara kwa mara kunaweza kukusaidia kula chakula kidogo na hivyo kupunguza uzito hasa kama utakunywa nusu saa au robo saa kabla ya chakula.
Kunywa nusu lita nusu saa kabla ya chakula na utaona umefanikiwa kula chakula kidogo na hivyo utaweza kupungua uzito kirahisi.
Hutakawia kuona faida ya mbinu hii kama utakuwa umeamua kila siku kunywa maji kila mara na zaidi kila nusu saa kabla ya chakula.
Tafadhali SHARE kwa ajili ya wengine

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am