Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Lissu awakumbusha viongozi wa dini kuzungumzia ukandamizwaji wa haki

Tundu Lissu awakumbusha viongozi wa dini kuzungumzia ukandamizaji haki
Uhakika media / 1 day ago

Tundu Lissu

Suleiman Kasei

MBUNGE wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), amewataka maaskofu, mashekhe, wachungaji, mapadri, wainjilisti, maimamu na wananchi kwa ujumla waamke kulaani vikali vitendo anavyodai vya ukandamizaji wa haki za binadamu.

Lissu ameyasema hayo ikiwa ni siku chache baada ya Mchungaji wa Kanisa la Kiinjilisti la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kilimanjaro Kati, Fred Njama kuhojiwa na Jeshi la Polisi mkoani humo.

Pamoja na Jeshi la Polisi kutosema sababu za kumkamata Mchungaji Njama, tukio la kukamatwa na kuhojiwa kiongozi huyo linakuja ikiwa ni siku chache baada ya kutoa taarifa ya kanisa lake kwa waamini ambapo aliaonisha changamoto mbalimbali zilizopo nchini kwa sasa.

Kwa mujibu wa video ambayo imesambaa mitandaoni ikimuonesha Mchungaji Njama anasema uchumi haujaimarika na umaskini unaendelea kuongezeka kwa nguvu.

“Umaskini umendelea kuongezeka kwa nguvu, tumeshuhudia biashara nyingi zikifungwa, wakulima wamekata tamaa na gharama za uzalishaji zimekuwa kubwa sana,” amesema.

Pia mchungaji huyo ameongeza kuwa serikali haitoi ruzuku ila wakati wa kuuza mazao wakulima hawana uhuru wauze wapi kwa bei gani, wafugaji pia wanazalisha kwa gharama kubwa.

Akizungumzia hali hiyo Lissu amesema kwa matukio ambayo yametokea takribani miaka miwili sasa ni wazi kuwa kila mwanajamii anapaswa kunyanyuka na kuachana na dhana ya kundi fulani kwani yote yameguswa.

“Maaskofu, wachungaji, mapadri, wainjilisti, mashehe, maimamu na kila aina ya kiongozi wetu wa kidini, waamke na kulaani vikali vitendo hivi vya ukandamizaji wa haki za binadamu za viongozi wa kiroho kutoa maoni yao hadharani na kukemea maovu ya utawala huu,” amesema.

Amefafanua kuwa ni wakati sasa wa waumini wao kuunga mkono na kushikamana nao na vyama vyetu vya siasa, taasisi za kiraia na kitaaluma na vyombo vya habari, navyo vipige kelele. 

“Kelele ya umma dhidi ya ukandamizaji ni kelele ya Mungu. Kimya mbele ya ukandamizaji ni kuunga mkono ukandamizaji,” amesema.

Amefafanua kuwa pamoja na ukweli kwamba aliyekamatwa ni kiongozi wa kidini, lakini sio viongozi wa kiroho peke yao wanaotakiwa kulaani ukandamizaji wa aina hii wa haki za binadamu na kuwa ni jambo la  kila mmoja wetu. 

Mbunge huyo amesema haki za binadamu ni za watu wote pamoja na viongozi wa kidini na ukandamizaji wa haki hizo kwa mtu mmoja ni ukandamizaji wa haki hizo kwa watu wote. 

Lissu ambaye yupo nchini Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi 32 akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma na watu wasiojulikana amesema ni miaka miwili iliyopita alisema hali hii inapaswa kupingwa na kila mwenye akili timamu lakini inawezekana hakueleweka.

“Tangu niyaseme maneno haya mahakamani Kisutu Juni 29 mwaka 2016, ni watu wangapi wameuawa, kupotezwa, kuumizwa, kukamatwa na kufunguliwa mashtaka ya 'uchochezi' au mengineyo ya ajabu ajabu,” amehoji. 

Amesema ni watu wangapi wamepoteza ajira zao, makazi yao, mali zao nyingine kutokana na matumizi ya ovyo ya madaraka ya utawala ulioko madarakani.

Kwa upande wake Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Rajab Katimba amesema kuna mahali taifa limekengeuka hali ambayo inatoa picha mbaya kwa jamii.

Katimba amesema viongozi wa Serikali wanapaswa kukaa na viongozi wale wa dini kuhakikisha jitihada za kusukuma gurudumu la maendeleo zinafanyika kwani kuwepo kwa mazingira ambayo yanaonekana kwa sasa sio afya nzuri kwa nchi.

“Tunatakiwa kukaa na kutafakari kinachoendelea nchini kwa sasa haya ambayo yanatokea sasa sio tamaduni zetu naamini tunapaswa kubadilika kwa maslahi ya Tanzania na Watanzania,” amesema.

Ameongeza kuwa viongozi wa dini na Serikali wanapaswa kufanya kazi pamoja kinyume cha hapo Taifa litaenda kusikohitajika kwani heshima ya viongozi wa dini inatakiwa kubakia pale pale.

Mwenyekiti wa jumiya hiyo Sheikh Mussa Kundecha, amewataka viongozi kutambua kuwa hakuna mtu mkamilifu hivyo wawe tayari kukosolewa pale inapobidi.

Kundecha amesema iwapo kila kiongozi ataishi katika misingi hiyo hakuna ambaye ataona kuwa ananyimwa raha na upande wowote huku akivitaka vyombo vya habari kutenda haki katika kuelimisha jamii.

Mtume Onesmo Ndegi, wa Kanisa la Living Waters Centre jijini Dar es Salaam, amesema taarifa hizo amezisikia ila hajapata undani wake na kwamba anataka kuzifanyia kazi ili aweze kuzungumza katika haki bila kumtuhumu mtu au taasisi.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am