Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Dawa 10 mbadala zinazo tibu shinikizo la chini la damu

Dawa mbadala 10 zinazotibu shinikizo la chini la damu
Published by fadhili on 08/09/2017
Dawa mbadala 10 zinazotibu shinikizo la chini la damu
Shinikizo la chini la damu hujulikana pia kama hypotension kwa Kiingereza. Ni hali ambayo shinikizo la damu ya mtu linakuwa chini sana na kusababisha dalili kama kizunguzungu, uchovu, udhaifu, kupumua kwa shida, kupungua kwa nuru ya macho nk
Utaambiwa una shinikizo la kawaida la damu kama vipimo vitasoma una 120/80 mm Hg.
Hata hivyo ikiwa vipimo vitasoma una
90/60 mm Hg au chini ya hapa, utaambiwa una shinikizo la chini la damu. Shinikizo la damu linapokuwa chini zaidi linaweza kupelekea msukumo ulio chini wa damu kwenye ogani kama ubongo, figo, na kwenye moyo.
Tatizo hili linaweza kusababishwa na vitu kama kupungua kwa maji mwilini, kulala sana, lishe duni, kushuka kwa wingi wa damu, matatizo ya moyo, ujauzito, homoni kutokuwa sawa na kadharika.
Baadhi ya dawa za hospitalini pia zinaweza kusababisha tatizo hili.
Unaposhughulika na shinikizo la chini la damu inashauriwa kuongeza matumizi ya chumvi na maji. Hata hivyo wasiliana na daktari wako wa karibu kabla kuamua lolote mwenyewe binafsi.
Kupona kabisa kwa tatizo hili kunategemea na aina hasa ya chanzo chake, hata hivyo unaweza kujaribu dawa mbadala zifuatazo ili kuzuia, kutibu au kupunguza dalili zake.
1. Maji chumvi
Maji yenye chumvi husaidia kutibu shinikizo la chini la damu sababu sodiamu iliyomo kwenye chumvi hupandisha juu shinikizo la damu. Usizidishe dawa hii hata hivyo sababu chumvi nyingi kuzidi ina madhara kiafya.
Matumizi: Changanya nusu kijiko cha chai cha chumvi ndani ya maji glasi moja (robo lita) na unywe mchanganyiko huu mara 1 au 2 kwa siku
2. Kahawa
Kunywa kikombe kimoja cha kahawa kunaweza pia kusaidia kupandisha shinikizo lako la damu kwa muda. Kama unapatwa na kushuka kwa shinikizo la damu mara kwa mara basi kunywa kikombe cha kahawa asubuhi au unywe wakati unakula cha mchana na cha jioni.
Hata hivyo usizidishe matumizi ya kahawa kwakuwa kahawa ina madhara mabaya kwa afya ya mwili kwa ujumla.
Vitu vingine ambavyo ni sawa na kahawa ni pamoja na cocoa, chai ya rangi, energy drinks zote, na soda nyeusi zote. Kuwa makini hata hivyo utumiavyo vitu hivi vikizidi vina madhara mwilini.
3. Zabibu kavu
Zabibu ni dawa ya asili inayotumika sana katika tiba za asili za India kutibu shinikizo la chini la damu kwa namna ya asili kabisa.
1. Loweka zabibu 30 mpaka 40 ndani ya kikombe cha maji kwa usiku mzima.
2. Asubuhi kabla ya kula wala kunywa chochote kula hizo zabibu moja baada ya nyingine na unywe pia maji yake
3. Fanya zoezi hili kila siku kwa majuma kadhaa hata mwezi.
4. Mrehani
Mrehani (basil) ni dawa nzuri ya kutibu shinikizo la chini la damu sababu ya kuwa na kiasi kingi cha vitamini C, magnesiamu na potasiamu, pia inasaidia kuweka sawa akili na kuondoa msongo wa mawazo (stress).
1. Chukua majani 10 mpaka 15 ya mrehani mbichi (freshi) na usage au utwange upate maji maji yake (juisi).
2. Ongeza asali kijiko kidogo kimoja ndani yake.
3. Kunywa mchanganyiko huu kila siku asubuhi ukiamka tu tumbo likiwa tupu.
Unaweza pia kuwa unatafuna tu moja kwa moja majani kadhaa ya mrehani kila siku asubuhi.
5. Lozi na maziwa
Hii ni dawa nyingine ya asili kwa ajili ya shinikizo la chini la damu.
1. Ziloweke lozi 5 mpaka 6 kwenye kikombe cha maji kwa usiku mmoja.
2. Asubuhi menya hizo lozi na uzisage.
3. Chukua hizo lozi ulizosaga na uweke ndani ya kikombe cha maziwa na uchemshe kwa dakika kadhaa. Kunywa kinywaji hiki kila siku asubuhi.
6. Juisi ya karoti na asali
Kuanza siku yako na juisi freshi ya karoti iliyochanganywa na asali ni njia rahisi ya kutibu shinikizo la chini la damu.
1. Chukua glasi moja ya juisi ya karoti
2. Ongeza vijiko vikubwa viwili vya asali ndani yake
3. Changanya vizuri na unywe yote asubuhi tumbo likiwa tupu na jioni glasi nyingine kwa majuma kadhaa
7. Juisi ya limau
Juisi ya limau ni nzuri sana katika kutibu shinikizo la juu la damu, lakini inaweza pia kutumika kutibu shinikizo la chini la damu hasa ikiwa hili shinikizo la chini la damu limesababishwa na upungufu wa maji mwilini (dehydration).
Katika kutibu shinikizo la chini la damu unaweza kuchanganya juisi ya limau (maji maji ya limau) na chumvi kidogo na sukari. Hii inasaidia kuupa nguvu mwili wako kwa kuhamasisha utendaji kazi wa ini na kusaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula.
Unaweza pia kuchukua juisi ya miwa ukiongeza maji maji ya limau kijiko kidogo kimoja na chumvi kidogo kwa ajili hii.
8. Tangawizi
Tangawizi ni dawa maarufu imekuwa ikitumika kutibu shinikizo la juu la damu pia shinikizo la chini la damu. Tangawizi ina vitu vingi mhimu ndani yake ikijumuisha viuavijasumu sambamba na kemikali mimea zenye nguvu sana kama ‘gingerol’, ‘shogaol’, na ‘zingerone’, ambazo zinaweza kusaidia kuwa sawa msukumo wa damu.
Kazi kubwa hasa ya tangawizi ni kuwa huifanya damu isigande kazi ambayo ni mhimu katika kuweka sawa shinikizo la damu.
Unahitaji:
Kijiko kikubwa kikubwa cha tangawizi mbichi iliyoparuzwa (grated)
Kikombe kimoja cha maji ya moto
Chemsha katika moto kwa dakika 12 hivi
Kisha ipua na uchuje
Ikipoa kidogo kunywa yote, fanya hivi mara 2 kwa siku kila siku
9. Maji ya kunywa
Hii ni moja ya dawa rahisi kabisa ya shinikizo la chini la damu. Maji ni mhimu kwa kila ogani ndani ya mwili iweze kufanya kazi zake sawa. Hivyo sababu kuu ya mtu kuwa na shinikizo la chini au hata la juu ni matokeo ya mishipa ya damu kutokuwa na vimiminika vya kutosha.
Kwa ujumla mishipa yako ya damu imeundwa kwa maji maji ya damu (serum) na seli za damu. Ile ukijikata unaona damu inatoka hivi yale huwa ni maji ambayo ndani yake ndiyo kuna seli za damu (blood cells).
Muda wowote maji yanapopungua kwenye mwili wako hata vipenyo vya mishipa yako navyo hupungua ukubwa wake jambo linaloleta kushuka kwa shinikizo la damu. Matatizo yote haya ni matokeo ya kutokunywa maji ya kutosha kila siku.
Kwahiyo ili kupandisha juu shinikizo la damu unahitaji kunywa zaidi maji sambamba na juisi nyingine za matunda au za mboga mboga kila siku.
10. Kupangilia chakula
Pamoja na kutumia dawa mbadala 9 hapo juu, bado unahitaji kuwa bize na mazoezi ya viungo kila siku ili kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu. Epuka mazoezi mazito na ya kunyanyua vyuma vizito sana.
Wasiliana pia na daktari wako ikiwa dawa zozote unazotumia za ugonjwa wowote sasa zinaweza kuwa zinasababisha shinikizo la chini la damu au la.
Pia ni mhimu kula mlo kamili kila siku. Kula lishe duni kunaweza kupelekea kuzalishwa kwa damu isiyo na afya inayoleta shinikizo la damu.
Upungufu wa baadhi ya vitamini hasa vitamini za kundi B na madini kunaweza pia kuleta shinikizo la chini la damu. Hivyo ili kudhibiti shinikizo la chini la damu unahitaji kula mlo sahihi kila siku.
Kula zaidi vyakula vyenye protini, vyenye vitamini B na C kwa wingi. Kula milo midogo midogo hata mitano kuliko kula miwili au mitatu lakini ya nguvu sana.
Acha vilevi vyovyote mara tu unapogundulika na shinikizo la chini la damu. Epuka pia vyakula vyenye wanga sana kama tambi, mikate, viazi, wali nk
Pendelea pia kutumia kitunguu swaumu hasa kibichi ukitafuna punje 2 kila unapoenda kulala kadharika glasi moja ya juisi ya ubuyu kutwa mara 1.
Kwa mawasiliano zaidi: WhatsApp +255769142586

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am