Ruka hadi kwenye maudhui makuu

mbinu za kukusaidia kufikia malengo ya mafanikio

Uhakika media 2 · 3 hours ago
Umbali uliopo kati ya malengo yako na mafanikio ni mrefu sana, na una vikwazo vingi sana, nafahamu fika ya kwamba hilo unalitambua vizuri sana.Umbali huo ambao upo baadhi ya watu ambao wana Mafanikio wameweka mikakati thabiti ambayo imewafanya wameweza kufanikiwa.

Pia kwa upande watu ambao hawajafanikiwa kwa kiwango cha juu na wao katika malengo yao wameweka mikakati, ila wengi wao hukata tamaa njiani katika utekelezaji wa mambo mbalimbali yatayowalete mafanikio.

Hali hiyo hutokea kwa sababu wengi wao hushidwa kuhimili changamoto ambazo hujitokeza katika safari hiyo ya kutoka katika malengo hadi Mafanikio.

Kama na wewe ni miongoni mwa watu ambao hukata tamaa katika safari yako ya kuelekea mafanikio, naomba nichukue nafasi hii kuweza kukaribisha katika makala haya ambapo tutazungumzia masuala ya kupanga malengo yako hadi kufikia mafanikio.

Kwani Wengi hujikuta wakishindwa wakiishia njiani katika safari yao ya mafanikio hii ni kutokana kutokujua namna ya kuzitambua mbinu za kukuza malengo hadi mafanikio.

1. Malengo ni lazima yaandikwe.
Malengo lazima uyaandike sehemu ambayo inaonekana, hapa ni maana ya kwamba uandike sehemu ambayo inaonekana, kufanya hivi kutakuwa kuna kutakufanya malengo hayo uwe unayakumbuka na kujua namna ya kuayatekeleza.

Unaweza ukayaandika malengo hayo kuyaweka katika simu yako katika (screen saver), kioo ambacho unakitumia kujitazama asubuhi na sehemu nyingine ambayo utayaona malengo hayo.

2. Weka vipaumbele katika malengo yako.
Inawezekana fika ukawa na malengo mengi, yaandike malengo hayo katika makundi matatu.
Kundi la kwanza jua yapi ni malengo ya muhimu yapi si malengo ya muhimu, yapi ni malengo ya haraka na yapi sio malengo, na tatu andika malengo ambayo sio ya muhimu sana.

Endapo utagawa malengo hayo utajua ni kipi kinatakiwa kuanza na kipi kinatakiwa kufuata na kwa muda gani.

3. Anza kwa kuanza na hatua ndogo.
Siku zote kama ilivyo ukuaji Wa kiumbe chochote chenye uhai huanza ukuaji wake katika hali ya chini. Kama ilivyo kwa kiumbe yeyote katika ukuaji hata katika ukuaji wa mafanikio yako huanza katika ngazi za chini.

Kitu cha msingi ni kuweza kupanua wigo mpana kwa ajili ya kupata mafanikio zaidi kwa kila jambo ambalo unalifanya. Na kwa kuwa mafanikio hayana ukomo hakikisha ya kwamba kila iitwayo leo unapata kiu ya kutaka kufanikiwa zaidi.

4. Malengo ni lazima yawe chanya.
Mara kadha watu huwa na ndoto nzuri sana, na pia wengi wao hupanga mambo mazuri kwa ajili ya utekelezaji wa ndoto hizo, ila changamoto kubwa ambayo huwa inakuja ni pale ambapo linakuja suala la utekelezaji wa jambo hilo.

Hapo sasa ndipo utakapoanza kumsikia mtu anasema aaah hivi nitaweza kweli, inatakiwa uondokane na kukata tamaa, vinginevyo kufanikiwa utaendelea kusikia kwa akina Donald Trump.

5.Malengo lazima yawe katika muda maalumu.
Ni lazima uweke muda kamili kwa ajili ya kutekeleza malengo yako, ifike mahali Malengo yako yafananishe na makampuni yanayohusika ujenzi kwani wao kabla ya kuanza kwa mradi huwa wanafanya mahesabu ili kujua mradi huo wa ujenzi utachukua muda gani mpaka ukamilike.

Ukiishi katika utaratibu Wa kuweka mbinu hiyo itakuwa ni rahisi kwako kutekeleza mambo ambayo unataka kutekeza. Kwa mfano lengo lako ni kujenga nyumba unaweza ukaandika katika lengo lako ya kwamba baada ya muda fulani inabidi uwe umekamilisha ujenzi huo.

Kupanga malengo bila kujua muda Wa kutekeleza malengo ni sawa na bure. Hivyo ni vyema ukajua ya kwamba muda ni mali katika kufanikisha malengo yako kwa wakati sahihi.

6. Malengo ni lazima yawe na mbinu za utekelezaji.
Watu wengi wana malengo ya kusema kwa mdomo tu. Lakini nikwambie ya kwamba ukitaka kufa maskini basi endelea na utaratibu huo Wa kuweka malengo mdomoni.

Kama kweli unataka kufanikiwa hakikisha ya kwamba malengo ambayo umejipangia umeyaandika na kuandika mbinu au njia kwa ajili ya utekelezaji wa malengo hayo.

Kufanya hivi kutakusaidia kujua jinsi ambavyo utayatekeleza malengo hayo ili kupata mafanikio. Kwa mfano kama malengo yako ni kujenga nyumba basi huna budi kuandika mbinu ambazo zitakusaidia kutengeza nyumba hiyo, pia hapa huenda sambamba na bajeti ya utekelezaji wa malengo yako.

7. Malengo ni lazima yapimike.
Kila malengo ambayo umejipangia Ni lazima yaweze kupimika. Kama nilivyoeleza hapo awali ya kwamba malengo ni lazima yawe na muda maalum kwa ajili ya utekelezaji.

Hivyo ni lazima upime malengo yako ni wapi ambapo umefikia? Katika muda ambao umepanga kuyatekeza malengo hayo je unahisi utafikia malengo hayo?

Pia uchunguzi yakinifu juu ya malengo yako ni lazima ufanyike ili kujua fursa na changamoto ambazo zimejitokeza katika kutekeleza malengo yako.

Mpaka kufikia hapa sina la ziada, tukutane siku nyingine.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni Published by fadhili on 17/11/2017 DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni. Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono 2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu 3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva 4. Ajali kwenye neva 5. Kunywa pombe kupita kiasi 6. Uvutaji wa sigara na bangi 7. Uchovu sugu 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara 9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu 10. Ugonjwa wa kisukari nk Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutok

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am