Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Madawa mbadala 6 ya kutibu ganzi ya mikono na miguu

Dawa mbadala 6 zinazotibu ganzi mikononi na miguuni
Published by fadhili on 17/11/2017
DAWA MBADALA 6 ZINAZOTIBU GANZI MIKONONI NA MIGUUNI
Ganzi mikononi na miguuni inamaanisha kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana sababu kunakuwa hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano rya moja kwa moja na ubongo.
Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana miaka ya hivi karibuni.
Kinachosababisha ganzi mwilini ni pamoja na:
1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono
2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu
3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva
4. Ajali kwenye neva
5. Kunywa pombe kupita kiasi
6. Uvutaji wa sigara na bangi
7. Uchovu sugu
8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara
9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu
10. Ugonjwa wa kisukari nk
Kwa kawaida ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote lakini onana na daktari mapema ikiwa inakutokea mara kwa mara na pia ikiwa inakutokea na kudumu kwa muda mrefu. Inaweza kuwa ni ishara ya ugonjwa fulani ambao unahitaji matibabu ya haraka.
Kuumwa ganzi kwenye miguu na mikono yako linaweza kuwa ni jambo linaloudhi sana hata hivyo hapa mimi leo nimekuandalia dawa za asili unazoweza kuzitumia kuondokana na tatizo hili.
Endelea kusoma …
Dawa mbadala zinazotibu tatizo la ganzi mwilini:
1. Massaji
Kufanya mazoezi ya massaji wakati unapopatwa na ganzi ni namna nzuri ya kutibu ganzi. Massaji inaongeza msukumo na mzunguko wa damu jambo ambalo mwisho ni tiba kwa tatizo la ganzi. Zaidi masaji inasaidia kusisimua neva na misuli na hivyo kuimarisha na kuongeza mzunguko wa damu kwa ujumla.
*Kwa matokeo ya uhakika weka mafuta ya nazi au ya zeituni au ya mharadali (mustard oil) kwenye viganja vya mikono yako .
*Pakaa sehemu unapopata ganzi
*Massaji maeneo hayo na mikono yako kwa dakika 5 mpaka 7 hivi
*Fanya mara 3 hata 5 kwa siku.
2. Mazoezi ya viungo
Mazoezi husaidia kuimarisha mzunguko wa damu na kuongeza oksijeni sehemu zote za mwili na hivyo kuzuia mwili kupata ganzi.
Mazoezi ndiyo namna pekee ya bure ya kujikinga na kujitibu na magonjwa mengi ikiwemo tatizo la mwili kupatwa na ganzi.
MAZOEZI MAALUMU KWA ANAYESUMBULIWA NA MIGUU KUWAKA MOTO GANZI AU ASIDI KUZIDI MWILINI
Unalala chali, nyoosha mikono chini. Kisha nyanyua mguu mmoja juu unyooke, shusha chini mguu na unyanyuwe wa pili hivyo hivyo juu kisha chini. Endelea hivyo hivyo kwa mara kumi kumi kwa round 5. Zoezi lichukuwe dk 10
Nyanyuka na ujipigie saluti mwenyewe ukianzia mkono wa kulia mara 15 hamia mkono wa kushoto mara 15 tena kwa round 5
Kisha simama, chuchumaa simama, chuchumaa simama, hivyo hivyo mara 15 kwa round 5
Pia unasimama wima, nyoosha mikono yote juu na uishushe mabegani. Hivyo hivyo mikono juu mikono mabegani mara 15 kwa round 5
Fanya hivi mara 4 mpaka 5 kwa wiki.
Mazoezi ya kukimbia, kuendesha baiskeli, kuogelea ni mazuri pia.
3. Bizari
Bizari au manjano ambayo hujulikana kwa kiingereza kama ‘Turmeric’ ina kitu mhimu ndani yake kijulikanacho kama ‘curcumin’ ambacho husaidia kuongeza msukumo wa damu sehemu yote ya mwili wako.
Pamoja na hiyo pia bizari husaidia kuondoa maumivu na hali ya kutokujisikia vizuri katika mwili wako.
Ongeza kijiko kidogo kimoja cha chai cha unga wa bizari ndani ya kikombe cha maziwa ya uvuguvugu ongeza kiasi kidogo cha asali na unywe kutwa mara 1.
Unaweza pia kutengeneza uji mzito (paste) wa bizari na maji na utumie kufanya massaji sehemu unapopata ganzi.
4. Mdalasini
Mdalasini una kemikali na viinilishe mbalimbali ikiwemo manganizi na potasiamu na vitamini nyingi za kundi B.
Faida zake za kiafya zinajumuisha pia kuongeza msukumo wa damu kwenye miguu na mikono yako na hivyo kusadia kutibu tatizo la ganzi. Wataalamu wa tiba asili wanashauri gramu 2 mpaka 4 za unga wa mdalasini zitumike kila siku kwa ajili ya kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu mwilini.
Changanya kijiko kidogo kimoja cha chai ya mdalasini ya unga katika glasi ya maji ya moto na unywe yote mara moja kwa siku.
Au changanya kijiko kimoja kidogo cha chai cha mdalasini ya unga na kijiko kidogo kingine cha asali na ulambe mchanganyiko huu kila siku asubuhi kwa wiki kadhaa.
Angalizo kuhusu mdalasini feki:
Kabla sijakuacha, ni mhimu sana nikueleweshe juu ya mdalasini hasa ambao hutumika kama dawa. Siyo kila mdalasini unaouona unaweza kukupa maajabu haya, mwingine ni sumu kabisa mwilini. Na watu wengi hawajuwi hili jambo.
(a) Ceylon cinnamon
Mdalasini ambao hutumika kama dawa hujulikana kwa kitaalamu kama ‘Ceylon cinnamon’ na kwa kawaida wenyewe huuzwa gharama sana. Huwa na radha tamu na harufu ya kuvutia zaidi, unatoka katika nchi ya Sri Lanka katika mmea ujulikanao kama Cinnamon Zeylanicum. Hujulikana pia kama mdalasini wa India.
Huwa na rangi ya kahawia (light brown), mwembamba na mlaini.
(b) Cassia cinnamon
Wakati ule ambao ni feki na ni sumu pia hujulikana kama ‘Cassia cinnamon’ ni mdalasini huu ambao katika baadhi ya nchi umepigwa marufuku kutumika wala kuingizwa nchini mwao. Hujulikana pia kama mdalasini wa China na wengine huuitwa Saigon.
Mdalasini huu unatoka katika nchi za China, Vietnam na Indonesia. Wenyewe huwa una joto zaidi na huwa na radha kali nay a kuwasha ukiutumia. Madhara yake ni pamoja na kudhuru Ini na figo ukitumika kwa kipindi kirefu.
Cassia cinnamon huuzwa bei rahisi sana na mwingi unaopatikana huko masokoni ni huu. Huwa na rangi inayokaribia na uweusi.
Kwa kawaida ni vigumu kutofautisha aina hizi mbili za mdalasini ukishakuwa tayari katika mfumo wa unga tofauti na ukiwa bado katika fimbo au magome. Mhimu tu ni ununuwe kutoka kwa mtu unayemuamini zaidi.
5. Kula zaidi vyakula vyenye vitamini B
Ili kuzuia ganzi mwilini hasa kwenye mikono na miguu ni mhimu kwamba unakula vyakula zaidi vyenye vitamini B kwa wingi hasa vitamini B6 na B12.
Vitamini hizi ni mhimu kwa ajili ya afya nzuri katika kuzipa neva uwezo wa kufanya kazi vizuri na upungufu wake unaweza kusababisha ganzi katika sehemu mbalimbali za mwili kama kwenye mikono, vidole, na miguu.
Vyakula hivyo ni pamoja na mayai (mayai ya kuku wa kienyeji), parachichi, nyama, maharage, samaki, maziwa, mtindi, mbegu mbegu nk
Unaweza pia kutumia vitamini B-complex mara 2 kwa siku kila siku. Kwa dozi sahihi zaidi muulize daktari wako wa karibu.
6. Ongeza matumizi ya magnesiamu
Usawa mdogo wa magnesiamu katika mwili ni moja ya sababu ya kutokea kwa ganzi katika sehemu mbalimbali za mwili. Magnesiamu ni madini mhimu katika kuwezesha ufanyaji kazi ulio mzuri wa neva za mwili na mzunguko mzuri wa damu mwilini.
Kula vyakula vyenye magnesiamu zaidi kama vile mboga majani zenye rangi ya kijani, mbegu mbegu, siagi ya karanga, soya, parachichi, ndizi, chokoleti nyeusi, na mtindi wenye mafuta kidogo.
Unaweza pia kutumia viinilishe vya magnesiamu gramu 350 kila siku ila ongea kwanza na daktari wako wa karibu.
Mambo mengine mhimu ya kuzingatia
1. Kuwa bize na mazoezi kila siku
2. Usikae muda mrefu kwenye kiti
3. Epuka chai ya rangi, kahawa, soda nyeusi na vinywaji vingine vyote vyenye kaffeina
4. Kula zaidi matunda na mboga za majani
5. Kunywa maji mengi kila siku kidogo kidogo kutwa nzima
6. Epuka sigara na bidhaa nyingine za tumbaku
7. Vaa viatu ambavyo ni saizi yako pia epuka viatu vyenye visigino virefu zaidi
8. Hakikisha una uzito sahihi na siyo uliozidi
Mawasiliano zaidi: WhatsApp +255769142586

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

PAKUA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI HAPA

KWA WALE WAPENZI WA PICHA ZENYE UJUMBE WA MAPENZI BASI HIZI HAPA Uhakika media 

Dawa 8 zinazo tibu kipanda uso kwa haraka

Uhakika media Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka Dawa za asili 8 zinazotibu kipanda uso kwa haraka   Kipanda uso ni ugonjwa gani?   Kipanda uso ni maumivu ya kichwa ambapo kichwa kinagonga kweli kweli na mara nyingine inaweza kuwa sehemu ya mbele au upande mmoja wa kichwa ndiyo unapatwa na maumivu haya.   Maumivu haya yanaweza kubaki kwa saa 4 mpaka saa 72. Vile vile dalili za ugonjwa huu zinatofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine.   Dalili za Kipanda Uso:   Unaweza kupata baadhi ya ishara za ugonjwa huu kama vile; 1. Kujisikia uvivu, 2. Kutapika, 3. Mauzauza, 4. Kusikia kelele sikioni nk. Wakati mwingine kabla ya kipanda uso watu wengine wanaweza kupatwa na miwasho, shingo nzito, kupiga miayo, kusikia njaa nk Sababu za kutokea kipanda uso mara nyingi ni pamoja na: 1. Mfadhaiko wa akili (stress) 2. Kelele nyingi kuzidi 3. Kuluka kula mlo 4. Pombe 5. Sigara 6. Shinikizo la chi

Dawa mbadala ya kutibu uke mkubwa au ulio legea

DAWA MBADALA ZINAZOTUMIKA KUREJESHA UKE MKUBWA AU ULIOLEGEA Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi. Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa. Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa. KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi. Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza. Watu wengine huamini kuwa mwanamke mw

SIMULIZI NZURI NA ZA KUSISIMUA sehemu ya 1

Simulizi: SINA WA KUMLAUMU (Siitaji Kurudi Nilipotoka) Sehemu ya 1 Uhakika media SIITAJI KURUDI NLIKOTOKA Mwandishi: SEID BIN SALIM SEHEMU YA KWANZA Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale. waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke ya

Hatua za kufuata wakati wa tendo la ndoa

USIJE UMBUKA, SOMA HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....! Uhakika media Wapnzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!   Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kus

NJIA 10 ZA KUTONGOZA KWA MACHO ZINAZO FANYA KAZI

Njia 10 za Kutongoza Kwa Macho Ambazo Hufanya Kazi Uhakika media   Je wataka kujifunza jinsi ya kutumia macho yako kupitisha ujumbe wa kuonyesha umevutiwa na mtu fulani? Kutumia macho kama mbinu ya kutongoza ni njia rahisi ya kupitisha ujumbe kutoka kwako hadi kwa yule unayemzimia kwa urahisi bila hata kutamka neno lolote. Mwanzo mchezo wa kutumia macho kama mbinu ya kutongoza huwa ina raha yake kiasi flani. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa ni rahisi kufahamu kiwango gani mtu amevutiwa nawe bila kuwauliza kuwatoa out. Pili ni kuwa uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unamjulisha unayemzimia na mapema ya kuwa umewavutia hivyo kujitayarisha na mapema iwapo atakubali kufanya maongezi na wewe. So ni mbinu zipi hizo unazoweza kutumia kumvutia unayempenda bila kuonekana kama fala? Njia za kutongoza kwa kutumia macho Utafanya nini iwapo umemuona yule aliyekupendeza katika mkahawa ama katika party ulioalikwa na marafiki zako? Kama hujui la kufanya basi tumia macho yako kumtongoza ili

VIDEO: Mbwembwe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra akamatwe na polisi' refa amtoa

VIDEO: Mbwembe za Joti aingia uwanjani kisa Samatta nusra abebwe na polisi, refa amtoa Uhakika media 1  · 12 hours ago Joti ambae ni msemaji wa team Samatta leo ameonyesha vituko vya aina yake ambapo imepelekea baadhi ya mashabiki kuachwa midomo wazi kwa kitendo cha kuingia uwanjani wakati mpira uneendelea baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambia kwenye eneo la hatari  TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

MBINU 10 ZA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME

Mbinu 10 za kuoongeza mbegu za kiume (sperm count) Mwanaume mwenye uwezo wa kuzalisha anahitaji kuwa na mbegu zisizopungua milioni 20, chochote chini ya hapa kinaweza kuwa sababu ya kutokutungisha ujauzito. Ikitokea umegundulika kuwa na mbegu chache, ni nyepesi sana na hazina nguvu za kukimbia vya kutosha basi makala hii itakupa maelezo juu ya mbinu 10 zinazoweza kukusaidia kuongeza uwingi wa mbegu zako bila gharama yoyote. Visababishi vya mbegu kuwa chache: Kuna vitu vingi vinavyoweza kusababisha tatizo la mbegu chache na ugumba kwa ujumla kwa wanaume, kwa bahati nzuri vingi ya vitu hivyo tunao uwezo wa kuvidhibiti kwa kupunguza matumizi yake. Vitu hivyo ni pamoja na: • Vifaa vya kieletroniki – Tafiti zimeonyesha vifaa vingi vya kisasa vya kieletroniki vinasababisha kushuka kwa wingi na ubora wa mbegu kwa wanaume wengi miaka ya sasa kwani mionzi yake hupelekea joto lisilohitajika katika mifuko ya mbegu za kiume. Vifaa hivi ni pamoja na simu na Kompyuta. Unashauriwa kutokuweka

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizo potea

Jinsi ya kurudisha hisia za mapenzi zilizopotea uhakika media 2  · 9 hours ago Tunaishi kwenye ulimwengu unaoenda kasi sana kiasi kwamba usipokuwa makini, unaweza kujikuta ukimpoteza mtu uliyempenda sana maishani kwa sababu tu ya kutojua namna ya kwenda naye sawa. Inafahamika kwamba mapenzi ni hisia lakini ni wachache wanaoweza kueleza jinsi ya kufanya hisia za mapenzi ziendelee kuwa hai. Siku hizi ndoa nyingi zinaendelea kuwepo kwa sababu ya kudra tu, unakuta mume na mke wanaishi kwa sababu ya mazoea tu lakini si kwa sababu ya mapenzi! Wengine wanakwambia kabisa, ‘mapenzi yalikuwa wakati tunaanzana’! Wanaishi tu ilimradi siku zinaenda, ilimradi wanawalea watoto lakini si kwa sababu ya upendo kati yao. Wengine wanafikia hatua hata ya kulala mzungu wa nne au kutengana vyumba kabisa! Au kwenda kulala vyumba vya watoto, watu haohao Kwa nje mnawaona kama wanapendana lakini kumbe ndani kuna ufa mkubwa kati yao, hakuna tena mapenzi kati yao. Cha ajabu, utakuta watu hawahawa am